< Mithali 20 >

1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
Wiyn is a letcherouse thing and drunkenesse is ful of noise; who euere delitith in these, schal not be wijs.
2 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
As the roryng of a lioun, so and the drede of the kyng; he that territh hym to ire, synneth ayens his owne lijf.
3 Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
It is onour to a man that departith hym silf fro stryuyngis; but fonned men ben medlid with dispisyngis.
4 Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
A slow man nolde ere for coold; therfor he schal begge in somer, and me schal not yyue to hym.
5 Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
As deep watir, so counsel is in the herte of a man; but a wijs man schal drawe it out.
6 Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
Many men ben clepid merciful; but who schal fynde a feithful man?
7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
Forsothe a iust man that goith in his simplenesse, schal leeue blessid sones aftir hym.
8 Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
A king that sittith in the seete of doom, distrieth al yuel bi his lokyng.
9 Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
Who may seie, Myn herte is clene; Y am clene of synne?
10 Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
A weiyte and a weiyte, a mesure and a mesure, euer eithir is abhomynable at God.
11 Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
A child is vndurstondun bi hise studies, yf his werkis ben riytful and cleene.
12 Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
An eere heringe, and an iye seynge, God made euere eithir.
13 Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
Nyle thou loue sleep, lest nedynesse oppresse thee; opene thin iyen, and be thou fillid with looues.
14 “Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
Ech biere seith, It is yuel, it is yuel; and whanne he hath go awey, thanne he schal haue glorie.
15 Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
Gold, and the multitude of iemmes, and a preciouse vessel, ben the lippis of kunnyng.
16 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Take thou awei the cloth of hym, that was borewe of an othere man; and for straungeris take thou awei a wed fro hym.
17 Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
The breed of a leesing is sweet to a man; and aftirward his mouth schal be fillid with rikenyng.
18 Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
Thouytis ben maad strong bi counselis; and bateils schulen be tretid bi gouernals.
19 Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
Be thou not medlid with him that schewith pryuetees, and goith gylefulli, and alargith hise lippis.
20 Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
The liyt of hym that cursith his fadir and modir, schal be quenchid in the myddis of derknessis.
21 Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
Eritage to which me haastith in the bigynnyng, schal wante blessing in the laste tyme.
22 Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
Seie thou not, Y schal yelde yuel for yuel; abide thou the Lord, and he schal delyuere thee.
23 Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
Abhomynacioun at God is weiyte and weiyte; a gileful balaunce is not good.
24 Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
The steppis of man ben dressid of the Lord; who forsothe of men mai vndurstonde his weie?
25 Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
Falling of man is to make auow to seyntis, and aftirward to withdrawe the vowis.
26 Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
A wijs kyng scaterith wickid men; and bowith a bouwe of victorie ouer hem.
27 Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
The lanterne of the Lord is the spirit of man, that sekith out alle the priuetees of the wombe.
28 Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
Merci and treuthe kepen a kyng; and his trone is maad strong bi mekenesse.
29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
The ful out ioiyng of yonge men is the strengthe of hem; and the dignyte of elde men is hoornesse.
30 Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.
The wannesse of wounde schal wipe aweie yuels, and woundis in the priuyere thingis of the wombe.

< Mithali 20 >