< Mithali 20 >

1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
Víno činí posměvače, a nápoj opojný nepokojného; pročež každý, kdož se kochá v něm, nebývá moudrý.
2 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
Hrůza královská jako řvání mladého lva; kdož ho rozhněvá, hřeší proti životu svému.
3 Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
Přestati od sváru jest to každému ku poctivosti, ale kdožkoli se do nich zapletá, blázen jest.
4 Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
Lenoch neoře pro zimu, pročež žebrati bude ve žni, ale nadarmo.
5 Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
Rada v srdci muže voda hluboká, muž však rozumný dosáhne jí.
6 Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
Větší díl lidí honosí se účinností svou, ale v pravdě takového kdo nalezne?
7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
Spravedlivý ustavičně chodí v upřímnosti své; blažení synové jeho po něm.
8 Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
Král sedě na soudné stolici, rozhání očima svýma všecko zlé.
9 Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
Kdo může říci: Očistil jsem srdce své? Èist jsem od hříchu svého?
10 Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
Závaží rozdílná a míra rozdílná, obé to ohavností jest Hospodinu.
11 Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
Po skutcích svých poznáno bývá také i pachole, jest-li upřímé a pravé dílo jeho.
12 Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
Ucho, kteréž slyší, a oko, kteréž vidí, obé to učinil Hospodin.
13 Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
Nemiluj snu, abys nezchudl, otevři oči své, a nasytíš se chlebem.
14 “Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
Zlé, zlé, říká ten, kdož kupuje, a odejda, tedy se chlubí.
15 Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
Zlato a množství perel, a nejdražší klínot jsou rtové umělí.
16 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Vezmi roucho toho, kterýž slíbil za cizího, a kdo za cizozemku, základ jeho.
17 Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
Chutný jest někomu chléb falše, ale potom ústa jeho pískem naplněna bývají.
18 Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
Myšlení radou upevňuj, a s opatrnou radou veď boj.
19 Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
Kdo vynáší tajnost, chodí neupřímě, pročež k lahodícímu rty svými nepřiměšuj se.
20 Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
Kdo zlořečí otci svému neb matce své, zhasne svíce jeho v temných mrákotách.
21 Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
Dědictví rychle z počátku nabytému naposledy nebývá dobrořečeno,
22 Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
Neříkej: Odplatím se zlým; očekávej na Hospodina, a vysvobodí tě.
23 Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
Ohavností jsou Hospodinu závaží rozdílná, a váhy falešné neoblibuje.
24 Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
Od Hospodina jsou krokové muže, ale člověk jak vyrozumívá cestě jeho?
25 Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
Osídlo jest člověku pohltiti věc posvěcenou, a po slibu zase toho vyhledávati.
26 Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
Král moudrý rozptyluje bezbožné, a uvodí na ně pomstu.
27 Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
Duše člověka jest svíce Hospodinova, kteráž zpytuje všecky vnitřnosti srdečné.
28 Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
Milosrdenství a pravda ostříhají krále, a milosrdenstvím podpírá se trůn jeho.
29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
Ozdoba mládenců jest síla jejich, a okrasa starců šediny.
30 Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.
Modřiny ran jsou lékařství při zlém, a bití vnitřnostem života.

< Mithali 20 >