< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Min son, vill du anamma mitt tal, och min bud när dig behålla,
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
Så låt din öron gifva akt på vishet, och böj ditt hjerta dertill med flit.
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
Ty om du far derefter med flit, och beder derom;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
Om du söker efter henne, såsom efter silfver, och letar efter henne, såsom efter en skatt;
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Så skall du förstå Herrans fruktan, och Guds kunskap finna.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Ty Herren gifver vishet, och utaf hans mun kommer vett och förstånd.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
Han låter dem redeligom väl gå, och beskärmar de fromma;
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Och bevarar dem som rätt göra, och bevarar sina heligas väg.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Då skall du förstå rättfärdighet, och dom; och fromhet, och allan godan väg.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Om vishet faller dig på hjertat, så att du gerna lärer,
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Så skall godt råd bevara dig, och förstånd skall gömma dig;
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
Att du icke råkar in uppå de ondas väg, eller ibland dem som tala det vrångt är;
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
Och öfvergifva den rätta vägen, och gå mörka stigar.
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
De der glädjas att göra illa, och äro glade uti sitt onda och vrångvisa väsende;
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Hvilke sin väg förvända, och följa villstigar;
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
Att du icke råkar in till ens annars hustru, och den icke din är, den slät ord gjfver;
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Och öfvergi! ver sins ungdoms herra, och förgäter sins Guds förbund;
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Ty hennes hus böjer sig till döden och hennes gånger till de förtappade;
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Alle de som ingå till henne, de komma intet igen, och fatta icke lifsens väg;
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
Att du må vandra på en god väg, och blifva på rätta stråtene.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Ty de rättfärdige skola bo i landena, och de fromme skola derinne blifva;
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Men de ogudaktige skola utu landena utrotade varda, och de föraktare skola derut förgjorde varda.

< Mithali 2 >