< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Hijo mío, si aceptas mis palabras, Y guardas mis mandamientos dentro de ti,
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
Eres de oído atento a la sabiduría, E inclinas tu corazón a la inteligencia,
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
Si invocas a la prudencia, Y al entendimiento alzas tu voz,
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
Si la procuras como a la plata, Y la rebuscas como a tesoros escondidos,
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Entonces entenderás el temor a Yavé, Y hallarás el conocimiento de ʼElohim.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Porque Yavé da la sabiduría. De su boca procede la ciencia y la inteligencia.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
Él atesora el acierto para los hombres rectos, Es escudo al que anda en integridad.
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Es el que guarda las sendas de la justicia, Y preserva el camino de sus santos.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Entonces entenderás la justicia y el derecho, La equidad y todo buen camino.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Cuando la sabiduría entre en tu corazón Y el conocimiento sea dulce a tu alma,
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Te guardará la discreción. Te preservará la prudencia
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
Para librarte del camino malo Del hombre que habla cosas perversas,
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
De los que abandonan los caminos rectos Para andar por sendas tenebrosas,
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
De los que gozan haciendo el mal, Y se alegran en las perversidades del vicio,
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Cuyas sendas son tortuosas, Y sus caminos extraviados.
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
Te librará de la mujer ajena, De la extraña que endulza sus palabras,
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Que abandona al compañero de su juventud Y olvida el Pacto de su ʼElohim.
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Su casa se inclina hacia la muerte, Sus sendas hacia el país de las sombras.
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Cuantos entran en ella no regresan, Ni retoman los senderos de la vida.
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
Para que sigas el buen camino Y guardes los senderos del justo.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Porque los rectos vivirán en la tierra, Y los de limpio corazón permanecerán en ella.
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Pero el perverso será cortado de la tierra, Y de ella serán desarraigados los transgresores.

< Mithali 2 >