< Mithali 2 >
1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Filho meu, se aceitares minhas palavras, e depositares em ti meus mandamentos,
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
Para fazeres teus ouvidos darem atenção à sabedoria, [e] inclinares teu coração à inteligência;
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
E se clamares à prudência, [e] à inteligência dirigires tua voz;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
Se tu a buscares como a prata, e a procurares como que a tesouros escondidos,
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Então entenderás o temor ao SENHOR, e acharás o conhecimento de Deus.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Porque o SENHOR dá sabedoria; de sua boca [vem] o conhecimento e o entendimento.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
Ele reserva a boa sabedoria para os corretos; [ele é] escudo para os que andam em sinceridade.
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Para guardar os caminhos do juízo; e conservar os passos de seus santos.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Então entenderás a justiça e o juízo, e a equidade; [e] todo bom caminho.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Quando a sabedoria entrar em teu coração, e o conhecimento for agradável à tua alma.
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
O bom senso te guardará, e o entendimento te preservará:
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
- Para te livrar do mau caminho, e dos homens que falam perversidades;
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
Que deixam as veredas da justiça para andarem pelos caminhos das trevas;
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
Que se alegram em fazer o mal, e se enchem de alegria com as perversidades dos maus;
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Cujas veredas são distorcidas, e desviadas em seus percursos.
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
- Para te livrar da mulher estranha, e da pervertida, [que] lisonjeia com suas palavras;
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Que abandona o guia de sua juventude, e se esquece do pacto de seu Deus.
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Porque sua casa se inclina para a morte, e seus caminhos para os mortos.
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Todos os que entrarem a ela, não voltarão mais; e não alcançarão os caminhos da vida.
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
- Para andares no caminho dos bons, e te guardares nas veredas dos justos.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Porque os corretos habitarão a terra; e os íntegros nela permanecerão.
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Porém os perversos serão cortados da terra, e os infiéis serão arrancados dela.