< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
בני אם-תקח אמרי ומצותי תצפן אתך
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
להקשיב לחכמה אזנך תטה לבך לתבונה
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
כי אם לבינה תקרא לתבונה תתן קולך
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
אם-תבקשנה ככסף וכמטמונים תחפשנה
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
אז--תבין יראת יהוה ודעת אלהים תמצא
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
כי-יהוה יתן חכמה מפיו דעת ותבונה
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
וצפן (יצפן) לישרים תושיה מגן להלכי תם
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
לנצר ארחות משפט ודרך חסידו ישמר
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
אז--תבין צדק ומשפט ומישרים כל-מעגל-טוב
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
כי-תבוא חכמה בלבך ודעת לנפשך ינעם
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
מזמה תשמר עליך תבונה תנצרכה
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
להצילך מדרך רע מאיש מדבר תהפכות
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
העזבים ארחות ישר-- ללכת בדרכי-חשך
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
השמחים לעשות רע יגילו בתהפכות רע
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
אשר ארחתיהם עקשים ונלוזים במעגלותם
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
להצילך מאשה זרה מנכריה אמריה החליקה
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
העזבת אלוף נעוריה ואת-ברית אלהיה שכחה
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
כי שחה אל-מות ביתה ואל-רפאים מעגלתיה
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
כל-באיה לא ישובון ולא-ישיגו ארחות חיים
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
למען--תלך בדרך טובים וארחות צדיקים תשמר
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
כי-ישרים ישכנו-ארץ ותמימים יותרו בה
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
ורשעים מארץ יכרתו ובוגדים יסחו ממנה

< Mithali 2 >