< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Mi sone, if thou resseyuest my wordis, `and hidist myn heestis anentis thee;
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
that thin eere here wisdom, bowe thin herte to knowe prudence.
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
For if thou inwardli clepist wisdom, and bowist thin herte to prudence;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
if thou sekist it as money, and diggist it out as tresours;
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
thanne thou schalt vndirstonde the drede of the Lord, and schalt fynde the kunnyng of God.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
For the Lord yyueth wisdom; and prudence and kunnyng is of his mouth.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
He schal kepe the heelthe of riytful men, and he schal defende hem that goen sympli.
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
And he schal kepe the pathis of riytfulnesse, and he schal kepe the weies of hooli men.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Thanne thou schalt vndirstonde riytfulnesse, and dom, and equytee, and ech good path.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
If wysdom entrith in to thin herte, and kunnyng plesith thi soule,
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
good councel schal kepe thee, and prudence schal kepe thee; that thou be delyuered fro an yuel weie,
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
and fro a man that spekith weiward thingis.
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
Whiche forsaken a riytful weie, and goen bi derk weies;
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
whiche ben glad, whanne thei han do yuel, and maken ful out ioye in worste thingis;
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
whose weies ben weywerd, and her goyingis ben of yuel fame.
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
That thou be delyuered fro an alien womman, and fro a straunge womman, that makith soft hir wordis;
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
and forsakith the duyk of hir tyme of mariage,
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
and hath foryete the couenaunt of hir God. For the hous of hir is bowid to deeth, and hir pathis to helle.
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Alle that entren to hir, schulen not turne ayen, nether schulen catche the pathis of lijf.
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
That thou go in a good weie, and kepe the pathis of iust men.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Forsothe thei that ben riytful, schulen dwelle in the lond; and symple men schulen perfitli dwelle ther ynne.
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
But vnfeithful men schulen be lost fro the loond; and thei that doen wickidli, schulen be takun awey fro it.

< Mithali 2 >