< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
My son, if you receive my words and treasure up my commandments with you,
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
make your ears pay attention to wisdom and incline your heart to understanding.
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
If you cry out for understanding and raise your voice for it,
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
if you seek it like you would seek silver and search for understanding as you would seek hidden treasures,
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
then you will understand the fear of Yahweh and you will find the knowledge of God.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
For Yahweh gives wisdom, from his mouth comes knowledge and understanding.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
He stores up sound wisdom for those who please him, he is a shield for those who walk in integrity,
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
he guards the paths of justice and he will preserve the way of those who are faithful to him.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Then you will understand righteousness, justice, and equity, and every good path.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
For wisdom will come into your heart, and knowledge will be pleasant to your soul.
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Discretion will watch over you, understanding will guard you.
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
They will rescue you from the way of evil, from those who speak perverse things,
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
who abandon the right paths and walk in the ways of darkness.
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
They rejoice when they do evil and delight in the perversities of evil.
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
They follow crooked paths, and using deception they hide their tracks.
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
Wisdom and discretion will save you from an adulterous woman, from an immoral woman and her flattering words.
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
She forsakes the companion of her youth and forgets the covenant of her God.
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
For her house leads down to death and her tracks will lead you to those in the grave.
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
All who go in to her will not return again and they will not find the paths of life.
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
So you will walk in the way of good people and follow the paths of righteous people.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
For those doing right will make a home in the land, and those with integrity will remain in it.
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
But the wicked will be cut off from the land, and the faithless will be cut off from it.

< Mithali 2 >