< Mithali 2 >
1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Mijn zoon! zo gij mijn redenen aanneemt, en mijn geboden bij u weglegt;
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
Om uw oren naar wijsheid te doen opmerken; zo gij uw hart tot verstandigheid neigt;
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
Ja, zo gij tot het verstand roept, uw stem verheft tot de verstandigheid;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
Zo gij haar zoekt als zilver, en naspeurt als verborgen schatten;
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Dan zult gij de vreze des HEEREN verstaan, en zult de kennis van God vinden.
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Want de HEERE geeft wijsheid; uit Zijn mond komt kennis en verstand.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
Hij legt weg voor de oprechten een bestendig wezen; Hij is een Schild dengenen, die oprechtelijk wandelen;
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Opdat zij de paden des rechts houden; en Hij zal den weg Zijner gunstgenoten bewaren.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Dan zult gij verstaan gerechtigheid, en recht, en billijkheden, en alle goed pad.
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Als de wijsheid in uw hart zal gekomen zijn, en de wetenschap voor uw ziel zal liefelijk zijn;
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Zo zal de bedachtzaamheid over u de wacht houden, de verstandigheid zal u behoeden;
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
Om u te redden van den kwaden weg, van den man, die verkeerdheden spreekt;
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
Van degenen, die de paden der oprechtheid verlaten, om te gaan in de wegen der duisternis;
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
Die blijde zijn in het kwaad doen, zich verheugen in de verkeerdheden des kwaden;
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Welker paden verkeerd zijn, en afwijkende in hun sporen;
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
Om u te redden van de vreemde vrouw, van de onbekende, die met haar redenen vleit;
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Die den leidsman harer jonkheid verlaat, en het verbond haars Gods vergeet;
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Want haar huis helt naar den dood, en haar paden naar de overledenen.
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Allen die tot haar ingaan, zullen niet wederkomen, en zullen de paden des levens niet aantreffen;
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
Opdat gij wandelt op den weg der goeden, en houdt de paden der rechtvaardigen.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Want de vromen zullen de aarde bewonen, en de oprechten zullen daarin overblijven;
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Maar de goddelozen zullen van de aarde uitgeroeid worden, en de trouwelozen zullen er van uitgerukt worden.