< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
Synu můj, přijmeš-li slova má, a přikázaní má schováš-li u sebe;
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
Nastavíš-li moudrosti ucha svého, a nakloníš-li srdce svého k opatrnosti;
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
Ovšem, jestliže na rozumnost zavoláš, a na opatrnost zvoláš-li;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
Budeš-li jí hledati jako stříbra, a jako pokladů pilně vyhledávati jí:
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Tehdy porozumíš bázni Hospodinově, a známosti Boží nabudeš;
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Nebo Hospodin dává moudrost, z úst jeho umění a opatrnost.
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
Chová upřímým dlouhověkosti, pavézou jest chodícím v sprostnosti,
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Ostříhaje stezek soudu; on cesty svatých svých ostříhá.
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Tehdy porozumíš spravedlnosti a soudu, a upřímosti i všeliké cestě dobré,
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Když vejde moudrost v srdce tvé, a umění duši tvé se zalíbí.
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Prozřetelnost ostříhati bude tebe, a opatrnost zachová tě,
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
Vysvobozujíc tě od cesty zlé, a od lidí mluvících věci převrácené,
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
Kteříž opouštějí stezky přímé, aby chodili po cestách tmavých,
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
Kteříž se veselí ze zlého činění, plésají v převrácenostech nejhorších,
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Jejichž stezky křivolaké jsou, anobrž zmotaní jsou na cestách svých;
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
Vysvobozujíc tě i od ženy postranní, od cizí, kteráž řečmi svými lahodí,
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Kteráž opouští vůdce mladosti své, a na smlouvu Boha svého se zapomíná;
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
K smrti se zajisté nachyluje dům její, a k mrtvým stezky její;
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Kteřížkoli vcházejí k ní, nenavracují se zase, aniž trefují na cestu života;
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
Abys chodil po cestě dobrých, a stezek spravedlivých abys ostříhal.
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Nebo upřímí bydliti budou v zemi, a pobožní zůstanou v ní;
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Bezbožní pak z země vyťati budou, a přestupníci vykořeněni budou z ní.

< Mithali 2 >