< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
我兒,你若接受我的話,把我的誡命存在心中,
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
側耳細聽智慧,專心尋求睿智;
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
你若呼求明哲,揚聲召尋睿智;
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
你若尋求她如尋求銀子,搜索她如搜索寶藏,
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
你必能領悟什麼是敬畏上主,也能明白什麼是認識天主。
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
因為,恩賜智慧的是上主,知識和睿智都出自他的口。
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
他給正直人保留了救援,又是行止成全者的護盾。
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
他護守正直人的行徑,他保衛虔誠者的道路;
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
這樣,你必能明瞭仁義和公平,明瞭正直和一切向善的道路。
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
如果智慧進入了你的心,智識成了你的喜樂,
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
慎思就必監護你,睿智也必防守你,
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
使你遠離邪道,遠離言詞荒謬的人:
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
即那些離棄正道,走上黑暗之途,
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
喜愛行惡,在邪惡中喜樂的人。
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
他們的道路彎曲不直,他們的行徑邪僻不正。
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
智慧將救你脫離淫婦,脫離甘言蜜語的娼妓。
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
她離棄了少年時的良友,忘記了她的天主的盟約;
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
為此,她的家屬趨向死亡,她的行徑通往黃泉;
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
凡行近她的人,沒有一個返回,再不會走上生路。
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
為此,你應走善人的道路,持守義人的行徑,
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
因為只有正直的人纔能住在地上,只有成全的人方得在那裏居留。
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
但是,作惡的人必由地上剷除,違法的人必由其中拔除。

< Mithali 2 >