< Mithali 19 >

1 Afadhali mtu maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama, kuliko mpumbavu ambaye midomo yake imepotoka.
טוב רש הולך בתמו מעקש שפתיו והוא כסיל׃
2 Sio vizuri kuwa na juhudi bila maarifa, wala kufanya haraka na kuikosa njia.
גם בלא דעת נפש לא טוב ואץ ברגלים חוטא׃
3 Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake hata hivyo moyo wake humkasirikia Bwana.
אולת אדם תסלף דרכו ועל יהוה יזעף לבו׃
4 Mali huleta marafiki wengi, bali rafiki wa mtu maskini humwacha.
הון יסיף רעים רבים ודל מרעהו יפרד׃
5 Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo hataachwa huru.
עד שקרים לא ינקה ויפיח כזבים לא ימלט׃
6 Wengi hujipendekeza kwa mtawala na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.
רבים יחלו פני נדיב וכל הרע לאיש מתן׃
7 Mtu maskini huepukwa na ndugu zake wote: Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani! Ingawa huwafuata kwa kuwasihi, hawapatikani popote.
כל אחי רש שנאהו אף כי מרעהו רחקו ממנו מרדף אמרים לא המה׃
8 Yeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe, yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.
קנה לב אהב נפשו שמר תבונה למצא טוב׃
9 Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo ataangamia.
עד שקרים לא ינקה ויפיח כזבים יאבד׃
10 Haistahili mpumbavu kuishi katika anasa, itakuwa vibaya kiasi gani kwa mtumwa kuwatawala wakuu.
לא נאוה לכסיל תענוג אף כי לעבד משל בשרים׃
11 Hekima ya mtu humpa uvumilivu, ni kwa utukufu wake kusamehe makosa.
שכל אדם האריך אפו ותפארתו עבר על פשע׃
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba, bali wema wake ni kama umande juu ya nyasi.
נהם ככפיר זעף מלך וכטל על עשב רצונו׃
13 Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye, naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha.
הות לאביו בן כסיל ודלף טרד מדיני אשה׃
14 Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Bwana.
בית והון נחלת אבות ומיהוה אשה משכלת׃
15 Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa.
עצלה תפיל תרדמה ונפש רמיה תרעב׃
16 Yeye ambaye hutii mafundisho huulinda uhai wake, bali yeye anayezidharau njia zake atakufa.
שמר מצוה שמר נפשו בוזה דרכיו יומת׃
17 Yeye amhurumiaye maskini humkopesha Bwana, naye atamtuza kwa aliyotenda.
מלוה יהוה חונן דל וגמלו ישלם לו׃
18 Mrudi mwanao, kwa maana katika hiyo kuna tumaini, usiwe mshirika katika mauti yake.
יסר בנך כי יש תקוה ואל המיתו אל תשא נפשך׃
19 Mtu mwenye kukasirika haraka ni lazima atapata adhabu yake, kama utamwokoa, itakubidi kufanya hivyo tena.
גרל חמה נשא ענש כי אם תציל ועוד תוסף׃
20 Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho, nawe mwishoni utakuwa na hekima.
שמע עצה וקבל מוסר למען תחכם באחריתך׃
21 Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu, lakini kusudi la Bwana ndilo litakalosimama.
רבות מחשבות בלב איש ועצת יהוה היא תקום׃
22 Lile mtu alionealo shauku ni upendo usio na mwisho, afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.
תאות אדם חסדו וטוב רש מאיש כזב׃
23 Kumcha Bwana huongoza kwenye uzima, kisha mtu hupumzika akiwa ameridhika, bila kuguswa na shida.
יראת יהוה לחיים ושבע ילין בל יפקד רע׃
24 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuupeleka kwenye kinywa chake!
טמן עצל ידו בצלחת גם אל פיהו לא ישיבנה׃
25 Mpige mwenye mzaha, naye mjinga atajifunza busara, mkemee mwenye ufahamu naye atapata maarifa.
לץ תכה ופתי יערם והוכיח לנבון יבין דעת׃
26 Yeye amwibiaye baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana aletaye aibu na fedheha.
משדד אב יבריח אם בן מביש ומחפיר׃
27 Mwanangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, utatangatanga mbali na maneno ya maarifa.
חדל בני לשמע מוסר לשגות מאמרי דעת׃
28 Shahidi mla rushwa hudhihaki hukumu na kinywa cha mtu mwovu humeza ubaya kwa upesi.
עד בליעל יליץ משפט ופי רשעים יבלע און׃
29 Adhabu zimeandaliwa kwa ajili ya wenye dhihaka na mapigo kwa ajili ya migongo ya wapumbavu.
נכונו ללצים שפטים ומהלמות לגו כסילים׃

< Mithali 19 >