< Mithali 18 >

1 Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.
Kas ar citiem kopā neturas, tas savu gribu tik meklē, un ir kavēklis visās lietās.
2 Mpumbavu hafurahii ufahamu, bali hufurahia kutangaza maoni yake mwenyewe.
Ģeķim netīk gudra valoda, bet tik vien atklāt savu paša sirdi.
3 Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia, pamoja na aibu huja lawama.
Bezdievīgam staigā līdz negods un ar apsmieklu kauns.
4 Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji, bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
Vārdi cilvēka mutē ir dziļš ūdens, un gudrības avots ir tekoša ūdens upīte.
5 Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.
Nav labi bezdievīga vaigu cienīt un nospiest taisno tiesā.
6 Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.
Ģeķa lūpas ieved ķildā, un viņa mute brēc pēc sitieniem.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.
Ģeķa mute sev pašai par postu, un viņa lūpas paša dvēselei par slazda valgu.
8 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Lišķa vārdi ir kā saldi kumosi un iet visai pie sirds.
9 Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.
Kas laisks pie darba, tas palaidņa brālis.
10 Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
Tā Kunga vārds ir stipra pils; tur taisnais glābjas un top izglābts.
11 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.
Bagātam manta ir viņa stiprā pils un viņam šķiet augsts mūris.
12 Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima.
Priekš bojāiešanas cilvēka sirds top lepna, bet pazemība ved godā.
13 Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake.
Kas atbild, pirms dzirdējis, tas tam par ģeķību un kaunu.
14 Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?
Vīra gars panes savas bēdas, bet kad gars izmisis, kas to var panest?
15 Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.
Prātīga sirds iemanto atzīšanu, un gudra auss meklē atzīšanu.
16 Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.
Dāvanas cilvēkam līdzina ceļu un viņu ved kungu priekšā.
17 Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi, hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.
Kas pirmais sūdz, tam taisnība; kad nu nāk viņa pretinieks, tad to tirda.
18 Kupiga kura hukomesha mashindano na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.
Mesli nobeidz ķildas un izšķir varenos.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.
Apkaitināts brālis ir cietāks nekā stipra pils, un ķilda nekā pils vārtu aizšaujamais.
20 Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake, atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.
No mutes augļiem ikkatrs savu vēderu pildīs, un viņa lūpu padoms to ēdinās.
21 Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi, nao waupendao watakula matunda yake.
Nāve un dzīvība stāv mēles galā; kā kurš runā, tā tam būs.
22 Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa Bwana.
Kas sievu atradis, tas atradis labumu un mantojis žēlastību no Tā Kunga.
23 Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.
Nabags runā lūgdamies, bet bagāts atbild bargi.
24 Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu, bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.
Citam daudz draugu uz postu; bet ir draugi, kas labāki nekā brālis.

< Mithali 18 >