< Mithali 17 >
1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Ліпший черствий кусок зо споко́єм, ніж дім, повний у́чти м'ясної зо сваркою.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
Раб розумний панує над сином безпутнім, і серед братів він поділить спа́док.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Для срі́бла — топи́льна посу́дина, а го́рно — для золота, Господь же серця випробо́вує.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Лиходій слухається уст безбожних, слухає неправдомо́в язика лиході́йного.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Хто сміється з убогого, той ображає свого Творця, хто радіє з нещастя, — не буде такий без вини.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Корона для ста́рших — ону́ки, а пишно́та дітей — їхні батьки́.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Не присто́йна безумному мова поважна, а тим більше шляхе́тному — мова брехли́ва.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Хабар в о́чах його власника́ — самоцві́т: до всьо́го, до чого пове́рнеться, буде щасти́ти йому́.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Хто шукає любови — провину ховає, хто ж про неї повто́рює, розго́нює дру́зів.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
На розумного більше впливає одне остере́ження, як на глупака́ сто ударів.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Злий шукає лише неслухня́ности, та вісник жорстокий на нього пошлеться.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Ліпше спітка́ти обезді́тнену ведмедицю, що кидається на люди́ну, аніж нерозумного в глупо́ті його.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Хто відплачує злом за добро, — не відступить лихе з його дому.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
Почин сварки — то про́рив води, тому перед ви́бухом сварки покинь ти її!
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
Хто оправдує несправедливого, і хто засуджує праведного, — оби́два вони Господе́ві оги́дні.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
На́що ті гроші в руці нерозумного, щоб мудрість купити, як мо́зку нема?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
Правдивий друг любить за всякого ча́су, в недолі ж він робиться братом.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Люди́на, позба́влена розуму, ру́читься, — пору́ку дає за друга свого.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
Хто сварку кохає, той любить гріх; хто ж підвищує уста свої, той шукає нещастя.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
Люди́на лукавого серця не зна́йде добра, хто ж лука́вить своїм язико́м, упаде в зло.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
Хто родить безумного, родить на смуток собі, і не поті́шиться батько безглуздого.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Серце радісне добре лікує, а пригно́блений дух сушить ко́сті.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Безбожний таємно бере хабара́, щоб зігнути путі правосу́ддя.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
З обличчям розумного — мудрість, а очі глупця́ — аж на кінці землі.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
Нерозумний син — смуток для батька, для своєї ж родительки — гі́ркість.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Не добре карати справедливого, бити шляхе́тних за щирість!
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
Хто слова́ свої стримує, той знає пізна́ння, і холоднокро́вний — розумна люди́на.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
І глупа́к, як мовчить, уважається мудрим, а як у́ста свої закриває — розумним.