< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Mejor es un bocado seco, y en paz, que la casa de contienda llena de sacrificios de fiesta.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
El siervo prudente se enseñoreará del hijo que deshonra, y entre los hermanos compartirá la herencia.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
El crisol para la plata, y la hornaza para el oro; mas el SEÑOR prueba los corazones.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
El malo está atento al labio inicuo; y el mentiroso escucha a la lengua maldiciente.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
El que escarnece al pobre, afrenta a su Hacedor; y el que se alegra en la calamidad ajena, no quedará sin castigo.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Corona de los viejos son los hijos de los hijos; y la honra de los hijos, sus padres.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
No conviene al loco la altilocuencia; ¡cuánto menos al príncipe el labio mentiroso!
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Piedra preciosa es el cohecho en ojos de sus dueños; a donde quiera que se vuelve, da prosperidad.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
El que cubre la prevaricación, busca el amor; mas el que reitera el asunto, aparta los amigos.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Aprovecha la reprensión en el entendido, más que cien azotes en el loco.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
El rebelde no busca sino mal; y mensajero cruel será enviado contra él.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Mejor es que se encuentre un hombre con una osa a la cual han robado sus cachorros, que con un loco en su locura.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
El que da mal por bien, no se apartará el mal de su casa.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
Soltar las aguas ( hablar precipitadamente ) es el principio de la contienda; pues, antes que se revuelva el pleito, déjalo.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
El que justifica al impío, y el que condena al justo, ambos por igual son abominación al SEÑOR.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
¿De qué sirve el precio en la mano del loco para comprar sabiduría, no teniendo corazón para entender?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
En todo tiempo ama el amigo; mas el hermano para la angustia es nacido.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
El hombre falto de entendimiento toca la mano, fiando a otro delante de su amigo.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
La prevaricación ama el que ama pleito; y el que alza su portada, quebrantamiento busca.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
El perverso de corazón nunca hallará bien; y el que revuelve con su lengua, caerá en mal.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
El que engendra al loco, para su tristeza lo engendra; y el padre del loco no se alegrará.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
El corazón alegre hará bien como una medicina; mas el espíritu triste seca los huesos.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
El impío toma dádiva en secreto para pervertir las veredas del derecho.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
En el rostro del entendido aparece la sabiduría; mas los ojos del loco manifiestan su locura hasta el cabo de la tierra.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
El hijo loco es enojo a su padre, y amargura a la que lo engendró.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Ciertamente no es bueno condenar al justo, ni herir a los príncipes por hacer lo recto.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
El que detiene sus palabras tiene sabiduría; y de espíritu valioso es el hombre entendido.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Aun el loco cuando calla, es contado por sabio; el que cierra sus labios es entendido.

< Mithali 17 >