< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Mejor es un bocado seco con tranquilidad, que una casa llena de fiestas con disputas.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
El siervo que trata con sabiduría gobernará sobre el hijo que causa vergüenza, y tendrá parte en la herencia entre los hermanos.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
El crisol es para la plata y el horno para el oro, pero Yahvé pone a prueba los corazones.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
El malhechor hace caso a los labios perversos. Un mentiroso da oídos a una lengua traviesa.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Quien se burla de los pobres reprocha a su Hacedor. El que se alegra de la calamidad no quedará impune.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Los hijos de los niños son la corona de los ancianos; la gloria de los niños son sus padres.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Un discurso excelente no es propio de un tonto, y mucho menos los labios mentirosos se ajustan a un príncipe.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
El soborno es una piedra preciosa a los ojos de quien lo da; a donde quiera que vaya, prospera.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
El que cubre una ofensa promueve el amor; pero quien repite un asunto separa a los mejores amigos.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Una reprimenda entra más profundamente en quien tiene entendimiento que cien latigazos a un tonto.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Un hombre malvado sólo busca la rebelión; por lo que se enviará un cruel mensajero contra él.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Que una osa despojada de sus cachorros se encuentre con un hombre, más que un tonto en su locura.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Quien recompensa el mal por el bien, el mal no saldrá de su casa.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
El comienzo de la contienda es como romper una presa, Por lo tanto, hay que detener la contienda antes de que se produzca una pelea.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
El que justifica al impío y el que condena al justo, ambos por igual son una abominación para Yahvé.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
¿Por qué hay dinero en la mano de un tonto para comprar sabiduría, ya que no tiene entendimiento?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
Un amigo ama en todo momento; y un hermano ha nacido para la adversidad.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Un hombre sin entendimiento golpea las manos, y se convierte en una garantía en presencia de su vecino.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
El que ama la desobediencia ama la contienda. El que construye una puerta alta busca la destrucción.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
El que tiene un corazón perverso no encuentra la prosperidad, y el que tiene una lengua engañosa cae en problemas.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
El que se convierte en padre de un tonto se apena. El padre de un tonto no tiene alegría.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Un corazón alegre es una buena medicina, pero un espíritu aplastado seca los huesos.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Un malvado recibe un soborno en secreto, para pervertir los caminos de la justicia.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
La sabiduría está ante el rostro del que tiene entendimiento, pero los ojos de un necio vagan hasta los confines de la tierra.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
El hijo insensato causa dolor a su padre, y la amargura a la que lo parió.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
También castigar al justo no es bueno, ni para azotar a los funcionarios por su integridad.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
El que ahorra sus palabras tiene conocimiento. El que es ecuánime es un hombre comprensivo.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Incluso el necio, cuando guarda silencio, es considerado sabio. Cuando cierra los labios, se cree que tiene criterio.

< Mithali 17 >