< Mithali 17 >
1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Boljši je suh košček in z njim spokojnost, kakor hiša polna klavnih daritev s prepirom.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
Moder služabnik bo imel vladarstvo nad sinom, ki povzroča sramoto in bo imel delež dediščine med brati.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Talilni lonec je za srebro in talilna peč za zlato, toda Gospod preizkuša srca.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Zloben storilec daje prednost nepravim ustnicam in lažnivec pazljivo prisluhne nespodobnemu jeziku.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Kdorkoli zasmehuje ubogega, graja njegovega Stvarnika in kdor je ob katastrofah vesel, ne bo nekaznovan.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Otrok otroci so krona starcem in slava otrok so njihovi očetje.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Odličen govor se ne spodobi bedaku, veliko manj lažnive ustnice princu.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Darilo je kakor dragocen kamen v očeh tistega, ki ga ima, kamor ga obrača, to uspeva.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Kdor taji prestopek, išče ljubezni, toda kdor ponavlja zadevo, ločuje prave prijatelje.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Opomin bolj prodira v modrega kakor sto udarcev z bičem v bedaka.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Hudoben človek išče samo upor, zato bo zoper njega poslan krut poslanec.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Naj medvedka, oropana svojih mladičev, sreča človeka, raje kakor bedak v svoji neumnosti.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Kdorkoli nagrajuje zlo za dobro, se zlo ne bo ločilo od njegove hiše.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
Začetek prepira je kakor kadar nekdo izpušča vodo, zato prenehaj s sporom, preden se vmešaš vanj.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
Kdor opravičuje zlobnega in kdor obsoja pravičnega, celo oba sta Gospodu ogabnost.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Zakaj je denarna vsota v bedakovi roki, da pridobi modrost, glede na to, da on nima srca za to?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
Prijatelj ljubi ob vseh časih in brat je rojen za stisko.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Človek brez razumevanja udarja v roke in postaja pôrok v prisotnosti svojega prijatelja.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
Kdor ljubi prestopek, ta ljubi prepir in kdor povišuje svoja velika vrata, išče uničenje.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
Kdor ima kljubovalno srce, ne najde dobrega in kdor ima sprevržen jezik, pada v vragolijo.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
Kdor zaplodi bedaka, to počne v svojo bridkost in oče bedaka nima radosti.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Veselo srce dela dobro, podobno kot zdravilo, toda zlomljen duh suši kosti.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Zloben človek iz naročja izvleče darilo, da izkrivlja poti sodbe.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Modrost je pred tistim, ki ima razumevanje, toda oči bedaka so na koncih zemlje.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
Nespameten sin je žalost svojemu očetu in grenkoba njej, ki ga je rodila.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Tudi kaznovati pravičnega ni dobro niti udariti prince zaradi nepristranskosti.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
Kdor ima spoznanje, prizanaša svojim besedam in razumevajoč človek je iz odličnega duha.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Celo bedak, ko molči, velja kot moder in kdor zapira svoje ustnice, je cenjen kot razumevajoč človek.