< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
平穏であって、ひとかたまりのかわいたパンのあるのは、争いがあって、食物の豊かな家にまさる。
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
賢いしもべは身持の悪いむすこを治め、かつ、その兄弟たちの中にあって、資産の分け前を獲る。
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
銀を試みるものはるつぼ、金を試みるものは炉、人の心を試みるものは主である。
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
悪を行う者は偽りのくちびるに聞き、偽りをいう者は悪しき舌に耳を傾ける。
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
貧しい者をあざける者はその造り主を侮る、人の災を喜ぶ者は罰を免れない。
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
孫は老人の冠である、父は子の栄えである。
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
すぐれた言葉は愚かな者には似合わない、まして偽りを言うくちびるは君たる者には似合わない。
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
まいないはこれを贈る人の目には幸運の玉のようだ、その向かう所、どこでも彼は栄える。
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
愛を追い求める人は人のあやまちをゆるす、人のことを言いふらす者は友を離れさせる。
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
一度の戒めがさとき人に徹するのは、百度の懲しめが愚かな人に徹するよりも深い。
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
悪しき者はただ、そむく事のみを求める、それゆえ、彼に向かっては残忍な使者がつかわされる。
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
愚かな者が愚かな事をするのに会うよりは、子をとられた雌ぐまに会うほうがよい。
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
悪をもて善に報いる者は、悪がその家を離れることがない。
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
争いの初めは水がもれるのに似ている、それゆえ、けんかの起らないうちにそれをやめよ。
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
悪しき者を正しいとする者、正しい者を悪いとする者、この二つの者はともに主に憎まれる。
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
愚かな者はすでに心がないのに、どうして知恵を買おうとして手にその代金を持っているのか。
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
友はいずれの時にも愛する、兄弟はなやみの時のために生れる。
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
知恵のない人は手をうって、その隣り人の前で保証をする。
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
争いを好む者は罪を好む、その門を高くする者は滅びを求める。
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
曲った心の者はさいわいを得ない、みだりに舌をもって語る者は災に陥る。
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
愚かな子を生む者は嘆きを得る、愚か者の父は喜びを得ない。
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
心の楽しみは良い薬である、たましいの憂いは骨を枯らす。
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
悪しき者は人のふところからまいないを受けて、さばきの道をまげる。
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
さとき者はその顔を知恵にむける、しかし、愚かな者は目を地の果にそそぐ。
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
愚かな子はその父の憂いである、またこれを産んだ母の痛みである。
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
正しい人を罰するのはよくない、尊い人を打つのは悪い。
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
言葉を少なくする者は知識のある者、心の冷静な人はさとき人である。
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
愚かな者も黙っているときは、知恵ある者と思われ、そのくちびるを閉じている時は、さとき者と思われる。

< Mithali 17 >