< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Un morceau de pain sec, avec la paix, vaut mieux qu'une maison pleine de viandes, avec des querelles.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
Le serviteur prudent dominera sur le fils qui fait honte, et il aura part à l'héritage avec les frères.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Le fourneau est pour éprouver l'argent, et le creuset pour l'or; mais c'est l'Éternel qui éprouve les cœurs.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Le méchant est attentif à la lèvre injuste, et le menteur écoute la langue qui calomnie.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Celui qui se moque du pauvre, déshonore celui qui l'a fait; et celui qui se réjouit d'un malheur, ne demeurera point impuni.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Les enfants des enfants sont la couronne des vieillards; et les pères sont la gloire de leurs enfants.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
La parole grave ne convient point à un insensé; combien moins la parole fausse aux principaux du peuple.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Le présent est comme une pierre précieuse aux yeux de ceux qui le reçoivent; de quelque côté qu'il soit tourné, il plaît.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Celui qui couvre les fautes, cherche l'amitié; mais celui qui en fait rapport, divise les meilleurs amis.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Une réprimande fait plus d'effet sur l'homme prudent, que cent coups sur l'insensé.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Le méchant ne cherche que des querelles; mais un messager cruel sera envoyé contre lui.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Mieux vaut rencontrer une ourse qui a perdu ses petits, qu'un fou dans sa folie.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Le mal ne quittera point la maison de celui qui rend le mal pour le bien.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
Commencer une querelle c'est ouvrir un passage à l'eau; avant qu'on en vienne à la dispute, retire-toi.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
Celui qui déclare juste le méchant, et celui qui déclare méchant le juste, sont tous deux en abomination à l'Éternel.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Que sert le prix dans la main d'un insensé pour acheter la sagesse, puisqu'il manque de sens?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
L'intime ami aime en tout temps, et il naîtra comme un frère dans la détresse.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Celui-là est dépourvu de sens, qui touche dans la main, et qui se rend caution envers son prochain.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
Celui qui aime les querelles, aime le mal; et celui qui élève trop son portail, veut qu'il croule.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
Le cœur pervers ne trouvera point le bonheur, et la langue double tombera dans le malheur.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
Celui qui a donné naissance à un insensé, en aura de l'ennui; et le père d'un fou ne se réjouira point.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Le cœur joyeux vaut un remède; mais l'esprit abattu dessèche les os.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Le méchant accepte le présent, pour renverser les voies de la justice.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
La sagesse est devant l'homme prudent; mais les yeux de l'insensé vont au bout de la terre.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
L'enfant insensé fait le chagrin de son père, et l'amertume de celle qui l'a enfanté.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Il n'est pas bon de condamner le juste à l'amende, ni de frapper les hommes honnêtes pour avoir fait ce qui est droit.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
L'homme retenu dans ses paroles connaît la prudence, et celui qui est d'un esprit froid, est un homme entendu.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
L'insensé même passe pour sage quand il se tait, et celui qui ferme ses lèvres est un homme intelligent.

< Mithali 17 >