< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Better a dry morsel, and peace therewith, than a house full of contentious sacrifices.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
A prudent servant, shall rule over a son who causeth shame, and, in the midst of brothers, shall he share the inheritance.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Fining-pot for silver, crucible for gold, but, he that trieth hearts, is Yahweh.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Discord, giveth heed to the aggrieving lip, —Falsehood, giveth ear to the destroying tongue.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
He that mocketh the poor, hath reproached his Maker, He that maketh merry at distress, shall not be held innocent.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
The crown of old men, consists of children’s children, and the adornment of children, is their fathers.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Unseemly in an unworthy man, is the lip of excellence, much more, in one of noble mind, the lip of falsehood.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
A gift, in the eyes of its owner, is, a stone of beauty, whithersoever it turneth, it bringeth prosperity.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
He that hideth a transgression, seeketh love, but, he that repeateth a matter, separateth intimate friends.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
A reproof sinketh more deeply into an intelligent man than a hundred stripes, into a dullard!
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Nothing less than rebellion, doth a wicked man seek, and, a relentless messenger, shall be sent out against him.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Let a bereaved bear encounter man, rather than a dullard, with his folly!
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
He that returneth evil for good, evil shall not depart from his house.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
A letting forth of water, is the beginning of strife, therefore, before it breaketh out, abandon, contention.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
He that justifieth the lawless, and he that condemneth the righteous, an abomination to Yahweh, are they, both.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Wherefore is there a price in the hand of a dullard? that he who is without sense, may acquire wisdom.
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
At all times, doth a friend love, and, a brother for distress, must be born.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
A man lacking sense, is one who striketh hands, giving security, before his neighbour.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
A lover of transgression, is one who loveth strife, he that heighteneth his door, seeketh grievous harm.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
The crooked in heart, shall not find good, and, he that is perverse with his tongue, shall fall into wickedness.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
He that begetteth a dullard, it is to his own grief, neither can the father of the base, rejoice.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
A joyful heart, worketh an excellent cure, —but, a stricken spirit, drieth up the bone.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
A bribe out of his bosom, doth a lawless man take, to pervert the ways of justice.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Before the face of the discerning, is wisdom, but, the eyes of a dullard, are in the ends of the earth.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
A vexation to his father, is the son that is a dullard, and a bitterness, to her that bare him.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Surely, to chastise the righteous, is not good, to smite the noble-minded for equity.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
Sparing of his words, is one who valueth knowledge, and, of a thoughtful spirit, is a man of intelligence.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Even a fool, holding his peace, is accounted, wise, —He that closeth his lips, [is thought] to have understanding.

< Mithali 17 >