< Mithali 17 >
1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Better is a dry morsel and quietness therewith, than an house full of feasting with strife.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
A servant that dealeth wisely shall have rule over a son that causeth shame, and shall have part in the inheritance among the brethren.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
The fining pot is for silver, and the furnace for gold: but the LORD trieth the hearts.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
An evil-doer giveth heed to wicked lips; [and] a liar giveth ear to a mischievous tongue.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Whoso mocketh the poor reproacheth his Maker: [and] he that is glad at calamity shall not be unpunished.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Children’s children are the crown of old men; and the glory of children are their fathers.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Excellent speech becometh not a fool: much less do lying lips a prince.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
A gift is [as] a precious stone in the eyes of him that hath it: whithersoever it turneth, it prospereth.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
He that covereth a transgression seeketh love: but he that harpeth on a matter separateth chief friends.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
A rebuke entereth deeper into one that hath understanding than an hundred stripes into a fool.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
An evil man seeketh only rebellion; therefore a cruel messenger shall be sent against him.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Let a bear robbed of her whelps meet a man, rather than a fool in his folly.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Whoso rewardeth evil for good, evil shall not depart from his house.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
The beginning of strife is [as] when one letteth out water: therefore leave off contention, before there be quarrelling.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
He that justifieth the wicked, and he that condemneth the righteous, both of them alike are an abomination to the LORD.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Wherefore is there a price in the hand of a fool to buy wisdom, seeing he hath no understanding?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
A friend loveth at all times, and a brother is born for adversity.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
A man void of understanding striketh hands, and becometh surety in the presence of his neighbour.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
He loveth transgression that loveth strife: he that raiseth high his gate seeketh destruction.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
He that hath a froward heart findeth no good: and he that hath a perverse tongue falleth into mischief.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
He that begetteth a fool [doeth it] to his sorrow: and the father of a fool hath no joy.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
A merry heart is a good medicine: but a broken spirit drieth up the bones.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
A wicked man taketh a gift out of the bosom, to pervert the ways of judgment.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Wisdom is before the face of him that hath understanding: but the eyes of a fool are in the ends of the earth.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
A foolish son is a grief to his father, and bitterness to her that bare him.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
Also to punish the righteous is not good, [nor] to smite the noble for [their] uprightness.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
He that spareth his words hath knowledge: and he that is of a cool spirit is a man of understanding.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Even a fool, when he holdeth his peace, is counted wise: when he shutteth his lips, he is [esteemed as] prudent.