< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Better is a piece of dry bread, and quiet therewith, than a house full of the sacrifices of contention.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
An intelligent servant will have rule over a son that bringeth shame, and among the brothers will he have part of the inheritance.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
The crucible is for silver, and the furnace for gold; but the Lord probeth the hearts.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
An evil-doer listeneth to unjust lips: falsehood giveth ear to a tongue that bringeth destruction.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Whoso mocketh the poor blasphemeth his Maker: he that is glad at calamities will not remain unpunished.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
The crown of old men are children's children; and the ornament of children are their fathers.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
High-toned language is not seemly to a worthless fool: and yet much less the language of falsehood to a noble.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
As a precious stone appeareth a bribe in the eyes of him that obtaineth it: whithersoever it turneth, it prospereth.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
He that covereth a transgression seeketh love; but he that repeateth a matter separateth confident friends.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
A reproof penetrateth more deeply into a wise man, than a hundred stripes into a fool.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Only rebellion doth a bad man seek: therefore a cruel messenger will be sent out against him.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
A man may meet a she-bear robbed of her whelps, but not a fool in his folly.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Whoso bestoweth evil in return for good—evil shall not depart from his house.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
As one letteth loose [a stream] of water, so is the beginning of strife: therefore before it be enkindled, leave off the contest.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
He that declareth the wicked innocent, and he that condemneth the righteous, yea, both of them are equally an abomination to the Lord.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Wherefore is the purchase-money in the hand of a fool to acquire wisdom, seeing he hath no sense?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
A friend loveth at all times, and as a brother is he born for [the time of] distress.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
A man void of sense pledgeth his hand, and becometh surety for his friend.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
He loveth transgression that loveth quarrel; and he that maketh high his door seeketh destruction.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
He that hath a froward heart will not find happiness; and he that hath a perverse tongue will fall into evil.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
He that begetteth a fool [doth it] to his sorrow; and the father of a worthless fool cannot have any joy.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
A merry heart causeth a healthy appearance of the countenance, but a depressed spirit drieth up the bones.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
A wicked man taketh a bribe out of the bosom, to pervert the paths of justice.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Wisdom is before him that hath understanding; but the eyes of a fool are at the ends of the earth.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
A foolish son is a vexation to his father, and bitterness to her that hath born him.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
To punish the just with a fine even is not good, nor to strike the noble [-hearted] for [their] equity.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
He that holdeth back his speeches hath knowledge; and he that is sparing of his spirit is a man of understanding.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Even a fool, when he keepeth silence, is counted wise: he that shutteth his lips [is esteemed] a man of understanding.

< Mithali 17 >