< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Bedre en tør Bid Brød med fred end Huset fuldt af Sul med Trætte.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
Klog Træl bliver Herre over dårlig Søn og får lod og del mellem brødre.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Digel til Sølv og Ovn til Guld, men den, der prøver Hjerter, er HERREN.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Den onde hører på onde Læber, Løgneren lytter til giftige Tunger.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Hvo Fattigmand spotter, håner hans Skaber, den skadefro slipper ikke for Straf.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
De gamles Krone er Børnebørn, Sønners Stolthed er Fædre.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Ypperlig Tale er ej for en Dåre, end mindre da Løgnfor den, som er ædel.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Som en Troldsten er Gave i Giverens Øjne; hvorhen den end vender sig, gør den sin Virkning.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Den, der dølger en Synd, søger Venskab, men den, der ripper op i en Sag, skiller Venner.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Bedre virker Skænd på forstandig end hundrede Slag på en Tåbe.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Den onde har kun Genstridigbed for, men et skånselsløst Bud er udsendt imod ham.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Man kan møde en Bjørn, hvis Unger er taget, men ikke en Tåbe udi hans Dårskab.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Den, der gengælder godt med ondt, fra hans Hus skal Vanheld ej vige.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
At yppe Strid er at åbne for Vand, hold derfor inde, før Strid bryder løs.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
At frikende skyldig og dømme uskyldig, begge Dele er HERREN en Gru.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Hvad hjælper Penge i Tåbens Hånd til at købe ham Visdom, når Viddet mangler?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
Ven viser Kærlighed når som helst, Broder fødes til Hjælp i Nød.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Mand uden Vid giver Håndslag og går i Borgen for Næsten.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
Ven af Kiv er Ven af Synd; at højne sin Dør er at attrå Fald.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
Ej finder man Lykke, når Hjertet er vrangt, man falder i Våde, når Tungen er falsk.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
Den, der avler en Tåbe, får Sorg, Dårens Fader er ikke glad.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Glad Hjerte er godt for Legemet, nedslået Sind suger Marv af Benene.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Den gudløse tager Gave i Løn for at bøje Rettens Gænge.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Visdom står den forstandige for Øje, Tåbens Blik er ved Jordens Ende.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
Tåbelig Søn er sin Faders Sorg, Kvide for hende, som fødte ham.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
At straffe den, der har Ret, er ilde, værre endnu at slå de ædle.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
Den, som har Kundskab tøjler sin Tale, Mand med Forstand er koldblodig.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Selv Dåren, der tier, gælder for viis, forstandig er den, der lukker sine Læber.

< Mithali 17 >