< Mithali 17 >

1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
Bedre en tør Bid Brød med fred end Huset fuldt af Sul med Trætte.
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
Klog Træl bliver Herre over daarlig Søn og faar lod og del mellem Brødre.
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
Digel til Sølv og Ovn til Guld, men den, der prøver Hjerter, er HERREN.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
Den onde hører paa onde Læber, Løgneren lytter til giftige Tunger.
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
Hvo Fattigmand spotter, haaner hans Skaber, den skadefro slipper ikke for Straf.
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
De gamles Krone er Børnebørn, Sønners Stolthed er Fædre.
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
Ypperlig Tale er ej for en Daare, end mindre da Løgn for den, som er ædel.
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
Som en Troldsten er Gave i Giverens Øjne; hvorhen den end vender sig, gør den sin Virkning.
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Den, der dølger en Synd, søger Venskab, men den, der ripper op i en Sag, skiller Venner.
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Bedre virker Skænd paa forstandig end hundrede Slag paa en Taabe.
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
Den onde har kun Genstridighed for, men et skaanselsløst Bud er udsendt imod ham.
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
Man kan møde en Bjørn, hvis Unger er taget, men ikke en Taabe udi hans Daarskab.
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
Den, der gengælder godt med ondt, fra hans Hus skal Vanheld ej vige.
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
At yppe Strid er at aabne for Vand, hold derfor inde, før Strid bryder løs.
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
At frikende skyldig og dømme uskyldig, begge Dele er HERREN en Gru.
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
Hvad hjælper Penge i Taabens Haand til at købe ham Visdom, naar Viddet mangler?
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
Ven viser Kærlighed naar som helst, Broder fødes til Hjælp i Nød.
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
Mand uden Vid giver Haandslag og gaar i Borgen for Næsten.
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
Ven af Kiv er Ven af Synd; at højne sin Dør er at attraa Fald.
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
Ej finder man Lykke, naar Hjertet er vrangt, man falder i Vaade, naar Tungen er falsk.
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
Den, der avler en Taabe, faar Sorg, Daarens Fader er ikke glad.
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Glad Hjerte er godt for Legemet, nedslaaet Sind suger Marv af Benene.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
Den gudløse tager Gave i Løn for at bøje Rettens Gænge.
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
Visdom staar den forstandige for Øje, Taabens Blik er ved Jordens Ende.
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
Taabelig Søn er sin Faders Sorg, Kvide for hende, som fødte ham.
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
At straffe den, der har Ret, er ilde, værre endnu at slaa de ædle.
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
Den, som har Kundskab tøjler sin Tale, Mand med Forstand er koldblodig.
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
Selv Daaren, der tier, gælder for viis, forstandig er den, der lukker sine Læber.

< Mithali 17 >