< Mithali 17 >
1 Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
乾餅一張而平安共食,勝於滿屋佳餚而互相爭吵。
2 Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
聰明的僕人必能管治任性的兒子,且可與弟兄們共分產業。
3 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
鍋煉銀,爐煉金,上主煉人心。
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
奸詐的人,愛聽胡言亂語;說謊的人,輕信是非長短。
5 Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
嘲笑窮人的是凌辱他的造主;幸災樂禍的,必不能脫免懲罰。
6 Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
孫兒是老人的冠冕,父親是兒女的光榮。
7 Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
優雅的言詞,不適宜於愚人;虛偽的狂語,更不宜於君王。
8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
賄賂在饋贈者眼中,有如寶石;不論他要轉向何方,無往不利。
9 Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
掩飾他人的過錯,可獲得友愛;屢念舊日的過惡,則離間友誼。
10 Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
對明智人一句指責,勝過對愚昧人百次杖擊。
11 Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
暴徒只求叛亂,但有殘酷使者,奉命前來對付。
12 Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
寧願遇見失掉幼子的母熊,不願逢著正在發狂的愚人。
13 Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
誰以怨報德,災禍必不離開他的家。
14 Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
爭論的開端,如水之破堤;在激辯之前,應極加制止。
15 Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
宣判罪人無罪,判定義人有罪:二者同為上主所憎惡。
16 Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
愚昧的人,既沒有頭腦,手執金錢買智慧,又何益之有﹖
17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
朋友平時常相愛,唯在難中見兄弟。
18 Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
常為人擊掌作保,實是個無知之徒。
19 Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
好爭辯的人,實喜愛罪過;高舉門戶的,必自趨滅亡。
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
誰存心欺詐,不會得幸福;誰搬弄是非,必陷於災禍。
21 Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
生糊塗孩子的,只有悲哀;糊塗人的父親,毫無樂趣。
22 Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
愉快的心,是良好的治療;神志憂鬱,能使筋骨枯萎。
23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
惡人在大衣下受賄賂,是為顛倒正義的判詞。
24 Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
精明的人,常面向智慧;愚者的眼,向地極呆望,
25 Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
愚昧的兒子,是他父親的痛苦,是他生母的憂傷。
26 Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
科罰無辜,已屬不當;杖責君子,更屬不義。
27 Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
智者必沉默寡言,達人必心神鎮定。
28 Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.
愚人不發言,亦可充作智者;若謹口慎言,亦可視為哲人。