< Mithali 15 >
1 Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.
柔和なる答は憤恨をとどめ厲しき言は怒を激す
2 Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
智慧ある者の舌は知識を善きものとおもはしめ 愚なる者の口はおろかをはく
3 Macho ya Bwana yako kila mahali, yakiwaangalia waovu na wema.
ヱホバの目は何處にもありて惡人と善人とを鑒みる
4 Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, bali ulimi udanganyao huponda roho.
温柔き舌は生命の樹なり 悸れる舌は霊塊を傷ましむ
5 Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.
愚なる者はその父の訓をかろんず 誡命をまもる者は賢者なり
6 Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa, bali mapato ya waovu huwaletea taabu.
義者の家には多くの資財あり 惡者の利潤には擾累あり
7 Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
智者のくちびるは知識をひろむ 愚なる者の心は定りなし
8 Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.
惡者の祭物はヱホバに憎まれ 直き人の祈は彼に悦ばる
9 Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.
惡者の道はヱホバに憎まれ 正義をもとむる者は彼に愛せらる
10 Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; yeye achukiaye maonyo atakufa.
道をはなるる者には厳しき懲治あり 譴責を惡む者は死ぬべし
11 Mauti na Uharibifu viko wazi mbele za Bwana: je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu! (Sheol )
陰府と況淪とはヱホバの目の前にあり 況て人の心をや (Sheol )
12 Mwenye mzaha huchukia maonyo; hatataka shauri kwa mwenye hekima.
嘲笑昔は誡めらるることを好まず また智慧ある者に近づかず
13 Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke, bali maumivu ya moyoni huponda roho.
心に喜樂あれば顔色よろこばし 心に憂苦あれば氣ふさぐ
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu.
哲者のこころは知識をたづね 愚なる者の口は愚をくらふ
15 Siku zote za wanaoonewa ni za taabu, bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu.
艱難者の日はことごとく惡く 心の懽べる者は恒に酒宴にあり
16 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana, kuliko mali nyingi pamoja na ghasia.
すこしの物を有てヱホバを畏るるは多の寳をもちて擾煩あるに愈る
17 Afadhali chakula cha mboga mahali palipo na upendo kuliko nyama ya ndama iliyonona pamoja na chuki.
蔬菜をくらひて互に愛するは肥たる牛を食ひて互に恨むるに愈る
18 Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.
憤ほり易きものは争端をおこし 怒をおそくする者は争端をとどむ
19 Njia ya mvivu imezibwa na miiba, bali njia ya mwenye haki ni barabara kuu.
惰者の道は棘の底に似たり 直者の途は平坦なり
20 Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
智慧ある子は父をよろこばせ 愚なる人はその母をかろんず
21 Upumbavu humfurahisha mtu ambaye hana akili, bali mtu mwenye ufahamu hushika njia iliyonyooka.
無知なる者は愚なる事をよろこび 哲者はその途を直くす
22 Mipango hushindwa kufanikiwa kwa ajili ya kukosa ushauri, bali kukiwa na washauri wengi hufanikiwa.
相議ることあらざれば謀計やぶる 議者おほければ謀計かならず成る
23 Mtu hupata furaha katika kutoa jibu linalofaa: je, ni zuri namna gani neno lililotoka kwa wakati wake!
人はその口の答によりて喜樂をう 言語を出して時に適ふはいかに善らずや
24 Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini. (Sheol )
哲人の途は生命の路にして上へ昇りゆく これ下にあるところの陰府を離れんが爲なり (Sheol )
25 Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.
ヱホバはたかぶる者の家をほろぼし 寡婦の地界をさだめたまふ
26 Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.
あしき謀計はヱホバに憎まれ 温柔き言は潔白し
27 Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu, bali yeye achukiaye rushwa ataishi.
不義の利をむさぼる者はその家をわづらはせ 賄賂をにくむ者は活ながらふべし
28 Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake, bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya.
義者の心は答ふべきことを考へ 惡者の口は惡を吐く
29 Bwana yuko mbali na waovu, bali husikia maombi ya wenye haki.
ヱホバは惡者に遠ざかり 義者の祈祷をききたまふ
30 Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni, nazo habari njema huipa mifupa afya.
目の光は心をよろこばせ 好音信は骨をうるほす
31 Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima atakuwa miongoni mwa wenye hekima.
生命の誡命をきくところの耳は智慧ある者の中間に駐まる
32 Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.
教をすつる者は自己の生命をかろんずるなり 懲治をきく者は聡明を得
33 Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima, nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.
ヱホバを畏るることは智慧の訓なり 謙遜は尊貴に先だつ