< Mithali 15 >
1 Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.
柔かい答は憤りをとどめ、激しい言葉は怒りをひきおこす。
2 Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
知恵ある者の舌は知識をわかち与え、愚かな者の口は愚かを吐き出す。
3 Macho ya Bwana yako kila mahali, yakiwaangalia waovu na wema.
主の目はどこにでもあって、悪人と善人とを見張っている。
4 Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, bali ulimi udanganyao huponda roho.
優しい舌は命の木である、乱暴な言葉は魂を傷つける。
5 Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.
愚かな者は父の教訓を軽んじる、戒めを守る者は賢い者である。
6 Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa, bali mapato ya waovu huwaletea taabu.
正しい者の家には多くの宝がある、悪しき者の所得には煩いがある。
7 Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
知恵ある者のくちびるは知識をひろめる、愚かな者の心はそうでない。
8 Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.
悪しき者の供え物は主に憎まれ、正しい者の祈は彼に喜ばれる。
9 Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.
悪しき者の道は主に憎まれ、正義を求める者は彼に愛せられる。
10 Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; yeye achukiaye maonyo atakufa.
道を捨てる者には、きびしい懲しめがあり、戒めを憎む者は死に至る。
11 Mauti na Uharibifu viko wazi mbele za Bwana: je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu! (Sheol )
陰府と滅びとは主の目の前にあり、人の心はなおさらである。 (Sheol )
12 Mwenye mzaha huchukia maonyo; hatataka shauri kwa mwenye hekima.
あざける者は戒められることを好まない、また知恵ある者に近づかない。
13 Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke, bali maumivu ya moyoni huponda roho.
心に楽しみがあれば顔色も喜ばしい、心に憂いがあれば気はふさぐ。
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu.
さとき者の心は知識をたずね、愚かな者の口は愚かさを食物とする。
15 Siku zote za wanaoonewa ni za taabu, bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu.
悩んでいる者の日々はことごとくつらく、心の楽しい人は常に宴会をもつ。
16 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana, kuliko mali nyingi pamoja na ghasia.
少しの物を所有して主を恐れるのは、多くの宝をもって苦労するのにまさる。
17 Afadhali chakula cha mboga mahali palipo na upendo kuliko nyama ya ndama iliyonona pamoja na chuki.
野菜を食べて互に愛するのは、肥えた牛を食べて互に憎むのにまさる。
18 Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.
憤りやすい者は争いをおこし、怒りをおそくする者は争いをとどめる。
19 Njia ya mvivu imezibwa na miiba, bali njia ya mwenye haki ni barabara kuu.
なまけ者の道には、いばらがはえしげり、正しい者の道は平らかである。
20 Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
知恵ある子は父を喜ばせる、愚かな人はその母を軽んじる。
21 Upumbavu humfurahisha mtu ambaye hana akili, bali mtu mwenye ufahamu hushika njia iliyonyooka.
無知な者は愚かなことを喜び、さとき者はまっすぐに歩む。
22 Mipango hushindwa kufanikiwa kwa ajili ya kukosa ushauri, bali kukiwa na washauri wengi hufanikiwa.
相はかることがなければ、計画は破れる、はかる者が多ければ、それは必ず成る。
23 Mtu hupata furaha katika kutoa jibu linalofaa: je, ni zuri namna gani neno lililotoka kwa wakati wake!
人は口から出る好ましい答によって喜びを得る、時にかなった言葉は、いかにも良いものだ。
24 Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini. (Sheol )
知恵ある人の道は上って命に至る、こうしてその人は下にある陰府を離れる。 (Sheol )
25 Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.
主は高ぶる者の家を滅ぼし、やもめの地境を定められる。
26 Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.
悪人の計りごとは主に憎まれ、潔白な人の言葉は彼に喜ばれる。
27 Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu, bali yeye achukiaye rushwa ataishi.
不正な利をむさぼる者はその家を煩らわせる、まいないを憎む者は生きながらえる。
28 Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake, bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya.
正しい者の心は答えるべきことを考える、悪しき者の口は悪を吐き出す。
29 Bwana yuko mbali na waovu, bali husikia maombi ya wenye haki.
主は悪しき者に遠ざかり、正しい者の祈を聞かれる。
30 Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni, nazo habari njema huipa mifupa afya.
目の光は心を喜ばせ、よい知らせは骨を潤す。
31 Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima atakuwa miongoni mwa wenye hekima.
ためになる戒めを聞く耳をもつ者は、知恵ある者の中にとどまる。
32 Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.
教訓を捨てる者はおのれの命を軽んじ、戒めを重んじる者は悟りを得る。
33 Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima, nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.
主を恐れることは知恵の教訓である、謙遜は、栄誉に先だつ。