< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.
מענה רך ישיב חמה ודבר עצב יעלה אף׃
2 Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
לשון חכמים תיטיב דעת ופי כסילים יביע אולת׃
3 Macho ya Bwana yako kila mahali, yakiwaangalia waovu na wema.
בכל מקום עיני יהוה צפות רעים וטובים׃
4 Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, bali ulimi udanganyao huponda roho.
מרפא לשון עץ חיים וסלף בה שבר ברוח׃
5 Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.
אויל ינאץ מוסר אביו ושמר תוכחת יערם׃
6 Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa, bali mapato ya waovu huwaletea taabu.
בית צדיק חסן רב ובתבואת רשע נעכרת׃
7 Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
שפתי חכמים יזרו דעת ולב כסילים לא כן׃
8 Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.
זבח רשעים תועבת יהוה ותפלת ישרים רצונו׃
9 Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.
תועבת יהוה דרך רשע ומרדף צדקה יאהב׃
10 Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; yeye achukiaye maonyo atakufa.
מוסר רע לעזב ארח שונא תוכחת ימות׃
11 Mauti na Uharibifu viko wazi mbele za Bwana: je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu! (Sheol h7585)
שאול ואבדון נגד יהוה אף כי לבות בני אדם׃ (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia maonyo; hatataka shauri kwa mwenye hekima.
לא יאהב לץ הוכח לו אל חכמים לא ילך׃
13 Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke, bali maumivu ya moyoni huponda roho.
לב שמח ייטב פנים ובעצבת לב רוח נכאה׃
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu.
לב נבון יבקש דעת ופני כסילים ירעה אולת׃
15 Siku zote za wanaoonewa ni za taabu, bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu.
כל ימי עני רעים וטוב לב משתה תמיד׃
16 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana, kuliko mali nyingi pamoja na ghasia.
טוב מעט ביראת יהוה מאוצר רב ומהומה בו׃
17 Afadhali chakula cha mboga mahali palipo na upendo kuliko nyama ya ndama iliyonona pamoja na chuki.
טוב ארחת ירק ואהבה שם משור אבוס ושנאה בו׃
18 Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.
איש חמה יגרה מדון וארך אפים ישקיט ריב׃
19 Njia ya mvivu imezibwa na miiba, bali njia ya mwenye haki ni barabara kuu.
דרך עצל כמשכת חדק וארח ישרים סללה׃
20 Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
בן חכם ישמח אב וכסיל אדם בוזה אמו׃
21 Upumbavu humfurahisha mtu ambaye hana akili, bali mtu mwenye ufahamu hushika njia iliyonyooka.
אולת שמחה לחסר לב ואיש תבונה יישר לכת׃
22 Mipango hushindwa kufanikiwa kwa ajili ya kukosa ushauri, bali kukiwa na washauri wengi hufanikiwa.
הפר מחשבות באין סוד וברב יועצים תקום׃
23 Mtu hupata furaha katika kutoa jibu linalofaa: je, ni zuri namna gani neno lililotoka kwa wakati wake!
שמחה לאיש במענה פיו ודבר בעתו מה טוב׃
24 Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini. (Sheol h7585)
ארח חיים למעלה למשכיל למען סור משאול מטה׃ (Sheol h7585)
25 Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.
בית גאים יסח יהוה ויצב גבול אלמנה׃
26 Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.
תועבת יהוה מחשבות רע וטהרים אמרי נעם׃
27 Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu, bali yeye achukiaye rushwa ataishi.
עכר ביתו בוצע בצע ושונא מתנת יחיה׃
28 Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake, bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya.
לב צדיק יהגה לענות ופי רשעים יביע רעות׃
29 Bwana yuko mbali na waovu, bali husikia maombi ya wenye haki.
רחוק יהוה מרשעים ותפלת צדיקים ישמע׃
30 Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni, nazo habari njema huipa mifupa afya.
מאור עינים ישמח לב שמועה טובה תדשן עצם׃
31 Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima atakuwa miongoni mwa wenye hekima.
אזן שמעת תוכחת חיים בקרב חכמים תלין׃
32 Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.
פורע מוסר מואס נפשו ושומע תוכחת קונה לב׃
33 Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima, nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.
יראת יהוה מוסר חכמה ולפני כבוד ענוה׃

< Mithali 15 >