< Mithali 13 >
1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye, bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.
智慧之子,聽從父親的教訓;輕狂的人,不聽任何人規勸。
2 Kutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema, bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri.
義人必飽嘗自己口舌的果實,惡人的慾望只有飽食強暴。
3 Yeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake, bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia.
謹口慎言,方能自保性命;信口開河,終必自取滅亡。
4 Mvivu hutamani sana na hapati kitu, bali nafsi ya mwenye bidii hutoshelezwa kikamilifu.
懶人雖常盼望,卻一無所得;勤勞的人,卻常如願以償。
5 Mwenye haki huchukia uongo, bali waovu huleta aibu na fedheha.
義人憎惡謊言,惡人令人可憎可惡。
6 Haki humlinda mtu mwadilifu, bali uovu humwangusha mwenye dhambi.
正義保衛行為正直的人,邪惡卻使罪人滅亡。
7 Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote; mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi.
有人自充富人,其實一貧如洗;有人佯作窮人,其實腰纏萬貫。
8 Utajiri wa mtu waweza kukomboa maisha yake, bali mtu maskini hasikii kitisho.
富人的錢財只是性命的贖價,窮人卻沒有這樣的威脅。
9 Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana, bali taa ya mwovu itazimwa.
義人的光明,必要高升;惡人的燈火,勢必熄滅。
10 Kiburi huzalisha magomvi tu, bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri.
傲慢只有引起爭端,虛心受教的人纔有智慧。
11 Fedha isiyo ya halali hupungua, bali yeye akusanyaye fedha kidogo kidogo huongezeka.
儻來之物,容易消逝;經久積存,日漸增多。
12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua, bali tumaini lililotimizwa ni mti wa uzima.
希望遲不兌現,令人心神煩惱;願望獲得滿足,像株生命樹。
13 Yeye anayedharau mafundisho anajiletea maangamizi, bali yeye anayeheshimu agizo hupewa tuzo.
誰輕視法令,必遭滅亡;誰敬畏誡命,必得安全。
14 Mafundisho ya mwenye busara ni chemchemi ya uzima, ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.
智慧人的教訓是生命的泉源,人可賴以脫免死亡的羅網。
15 Ufahamu mzuri hupata upendeleo, bali njia ya asiye mwaminifu ni ngumu.
明哲的規勸,使人蒙恩,殘暴人的舉止,粗魯蠻橫。
16 Kila mwenye busara hutenda kwa maarifa, bali mpumbavu hudhihirisha upumbavu wake.
精明的人,常按理智行事;愚昧的人,只自誇其糊塗。
17 Mjumbe mwovu huanguka kwenye taabu, bali mjumbe mwaminifu huleta uponyaji.
奸妄的使者,使人陷於災禍;忠誠的使者,給人帶來安和。
18 Yeye anayedharau maonyo hupata umaskini na aibu, bali yeye anayekubali maonyo huheshimiwa.
拒絕規勸的,必遭貧苦羞辱;接受懲戒的,反要受人尊敬。
19 Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi, bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya.
願望獲得滿足,能使心靈愉快;遠離邪惡,卻為愚昧人所深惡。
20 Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima, bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara.
與智慧人往來,可成智慧人;與愚昧人作伴,必受其連累。
21 Balaa humwandama mtenda dhambi, bali mafanikio ni thawabu kwa mwenye haki.
惡運追蹤罪人,義人卻得善報。
22 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi, bali mali ya wenye dhambi imehifadhiwa kwa ajili ya wenye haki.
善人為子子孫孫留下產業,罪人的財富是為義人積蓄。
23 Shamba la mtu maskini laweza kuzalisha chakula kingi, bali dhuluma hukifutilia mbali.
窮人開墾的田地,生產大量食物;誰若缺乏正義,定不免於滅亡。
24 Yeye aizuiaye fimbo yake hampendi mwanawe, bali yeye ampendaye huwa mwangalifu kumwadibisha.
不肯使用棍杖的人,實是恨自己的兒子;真愛兒子的人,必時加以懲罰。
25 Mwenye haki hula mpaka akaridhisha moyo wake, bali tumbo la mwovu hutaabika kwa njaa.
義人必得飽食,惡人無以果腹。