< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
EL que ama la corrección ama la sabiduría: mas el que aborrece la reprensión, es ignorante.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
El bueno alcanzará favor de Jehová: mas él condenará al hombre de malos pensamientos.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
El hombre no se afirmará por medio de la impiedad: mas la raíz de los justos no será movida.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
La mujer virtuosa corona es de su marido: mas la mala, como carcoma en sus huesos.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Los pensamientos de los justos son rectitud; [mas] los consejos de los impíos, engaño.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Las palabras de los impíos son para acechar la sangre: mas la boca de los rectos los librará.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
[Dios] trastornará á los impíos, y no serán más: mas la casa de los justos permanecerá.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Según su sabiduría es alabado el hombre: mas el perverso de corazón será en menosprecio.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Mejor es el que es menospreciado y tiene servidores, que el que se precia, y carece de pan.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
El justo atiende á la vida de su bestia: mas las entrañas de los impíos son crueles.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
El que labra su tierra, se hartará de pan: mas el que sigue los vagabundos es falto de entendimiento.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Desea el impío la red de los malos: mas la raíz de los justos dará [fruto].
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
El impío es enredado en la prevaricación de sus labios: mas el justo saldrá de la tribulación.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
El hombre será harto de bien del fruto de su boca: y la paga de las manos del hombre le será dada.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
El camino del necio es derecho en su opinión: mas el que obedece al consejo es sabio.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
El necio luego al punto da á conocer su ira: mas el que disimula la injuria es cuerdo.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
El que habla verdad, declara justicia; mas el testigo mentiroso, engaño.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Hay quienes hablan como [dando] estocadas de espada: mas la lengua de los sabios es medicina.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
El labio de verdad permanecerá para siempre: mas la lengua de mentira por un momento.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Engaño hay en el corazón de los que piensan mal: mas alegría en el de los que piensan bien.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Ninguna adversidad acontecerá al justo: mas los impíos serán llenos de mal.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Los labios mentirosos son abominación á Jehová: mas los obradores de verdad su contentamiento.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
El hombre cuerdo encubre la ciencia: mas el corazón de los necios publica la necedad.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
La mano de los diligentes se enseñoreará: mas la negligencia será tributaria.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
El cuidado congojoso en el corazón del hombre, lo abate; mas la buena palabra lo alegra.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
El justo hace ventaja á su prójimo: mas el camino de los impíos les hace errar.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
El indolente no chamuscará su caza: mas el haber precioso del hombre [es] la diligencia.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
En el camino de la justicia está la vida; y la senda de su vereda no es muerte.

< Mithali 12 >