< Mithali 12 >
1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Si amas el conocimiento, amarás la disciplina. ¡Todo el que aborrece la corrección es un necio!
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
El Señor bendice a los que hacen el bien, pero condena a los que conspiran para hacer el mal.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
La maldad no brinda seguridad, pero los que viven en justicia tienen sus raíces profundas y no serán removidos.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Una buena esposa es corona para su esposo, pero la mujer que trae vergüenza es como descomposición en sus huesos.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Las personas que hacen el bien, hacen planes justos, pero el consejo de los malvados es engañoso.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Las palabras de los malvados son como una emboscada con violencia, pero las palabras de las personas honestas los salvarán.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Los malvados son destriudos y olvidados. Pero la familia de los que hacen el bien permanece firme.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Las personas son estimadas cuando hablan con sensatez, pero los que tienen mentes perversas son aborrecidos.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Mejor es ser humilde y trabajar para ti mismo, que ser un hombre jactancioso y no tener nada para comer.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Los justos cuidan de sus animales, pero el cuidado de los malvados es crueldad.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Si cultivas la tierra, tendrás abundancia de dinero, pero si vas detrás de cosas inútiles, eres un tonto.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Las personas malvadas buscan el grano robado, pero las personas justas lo producen ellas mismas.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Los malvados quedan atrapados por sus propias palabras pecaminosas, pero las personas que hacen el bien se libran de los problemas.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Tus palabras te traerán recompensa, y tu trabajo regresará a bendecirte.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Los necios creen que van por el camino correcto, pero si eres sabio escucharás el consejo.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Los necios se enojan con facilidad; pero si eres prudente, ignorarás los insultos.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Quien dice la verdad es honesto, pero un testigo falso dirá mentiras.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Las palabras apresuradas pueden ser tan cortantes como un cuchillo, pero las palabras de los sabios traen sanidad.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Las palabras de verdad duran para siempre, pero las mentiras se olvidan pronto.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
En la mente de los que maquinan maldad solo hay engaño; pero los que piensan en hacer el bien viven con alegría.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
A los que hacen el bien no les pasara ningún mal, pero los malvados están llenos de problemas.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
El Señor aborrece a los mentirosos, pero se alegra con los fieles.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Si eres prudente, no presumes de tu conocimiento; pero los tontos anuncian su estupidez.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
El trabajo duro aporta liderazgo, pero la pereza trae esclavitud.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Si vives con ansiedad, te sentirás sobrecargado; pero una palabra de aliento te reconfortará.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Las personas que hacen el bien cuidan de sus amigos, pero la forma en que viven los malvados lleva a sus amigos a la perdición.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Los perezosos no atrapan su presa, pero si trabajas duro te volverás rico.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
El camino de los justos lleva a la vida, nunca te conducirá a la muerte.