< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Den som elsker tukt, elsker kunnskap; men den som hater refselse, er dum.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Den gode får nåde hos Herren, men den svikefulle mann fordømmer han.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Ugudelighet hjelper intet menneske til å stå støtt, men de rettferdiges rot rokkes ikke.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
En god hustru er sin manns krone, men en dårlig er som råttenhet i hans ben.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
De rettferdige tenker bare på det som rett er; de ugudeliges råd er svik.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
De ugudelige taler alltid om å lure efter blod, men de opriktiges munn frelser dem.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
De ugudelige kastes over ende, og så er de ikke mere; men de rettferdiges hus står fast.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
En mann roses alt efter som han har forstand, men den hvis hjerte er forvendt, blir til forakt.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Bedre er en småkårsmann som har en tjener, enn en som vil være storkar, men ikke har brød.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Den rettferdige har omsorg for sin buskap, men den ugudeliges hjerte er hårdt.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Den som dyrker sin jord, mettes med brød; men den som jager efter tomme ting, er uten forstand.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Den ugudelige attrår det som er en snare for de onde; men de rettferdige gir Gud fast rot.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
I lebenes synd ligger en ond snare, men den rettferdige kommer ut av trengsel.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Av sin munns frukt mettes en mann med godt, og hvad et menneskes hender har gjort, det gjengjeldes ham.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Dårens vei er rett i hans egne øine, men den som hører på råd, er vis.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Dårens vrede blir kjent samme dag, men den som skjuler krenkelser, er klok.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Den som er ærlig i sine ord, taler sannhet, men et falskt vidne taler svik.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Mange taler tankeløse ord, som stikker likesom sverd; men de vises tunge er lægedom.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Sannhets lebe blir fast for all tid, men falskhets tunge bare et øieblikk.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Det er svik i deres hjerte som smir ondt; men de som råder til fred, får glede.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Det rammer ikke den rettferdige noget ondt, men de ugudelige får ulykke i fullt mål.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Falske leber er en vederstyggelighet for Herren, men de som går frem med ærlighet, er ham til velbehag.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Et klokt menneske skjuler det han vet, men dårers hjerte roper ut sin dårskap.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
Den flittiges hånd kommer til å styre, men lathet blir træl.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Sorg i en manns hjerte trykker det ned, men et godt ord gleder det.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Den rettferdige veileder sin næste, men de ugudeliges vei fører dem vill.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Lathet steker ikke sin fangst, men flid er en kostelig skatt for et menneske.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
På rettferds sti er liv, og en ryddet vei fører ikke til døden.

< Mithali 12 >