< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Qui diligit disciplinam, diligit scientiam: qui autem odit increpationes, insipiens est.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Qui bonus est, hauriet gratiam a Domino: qui autem confidit in cogitationibus suis, impie agit,
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Non roborabitur homo ex impietate: et radix iustorum non commovebitur.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Mulier diligens, corona est viro suo: et putredo in ossibus eius, quæ confusione res dignas gerit.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Cogitationes iustorum iudicia: et consilia impiorum fraudulenta:
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Verba impiorum insidiantur sanguini: os iustorum liberabit eos.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Verte impios, et non erunt: domus autem iustorum permanebit.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Doctrina sua noscetur vir: qui autem vanus et excors est, patebit contemptui.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Melior est pauper et sufficiens sibi, quam gloriosus et indigens pane.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Novit iustus iumentorum suorum animas: viscera autem impiorum crudelia.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Qui operatur terram suam, satiabitur panibus: qui autem sectatur otium, stultissimus est. Qui suavis est in vini demorationibus, in suis munitionibus relinquit contumeliam.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Desiderium impii munimentum est pessimorum: radix autem iustorum proficiet.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Propter peccata labiorum ruina proximat malo: effugiet autem iustus de angustia.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
De fructu oris sui unusquisque replebitur bonis, et iuxta opera manuum suarum retribuetur ei.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Via stulti recta in oculis eius: qui autem sapiens est, audit consilia.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Fatuus statim indicat iram suam: qui autem dissimulat iniuriam, callidus est.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Qui quod novit loquitur, index iustitiæ est: qui autem mentitur, testis est fraudulentus.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Est qui promittit, et quasi gladio pungitur conscientiæ: lingua autem sapientium sanitas est.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Labium veritatis firmum erit in perpetuum: qui autem testis est repentinus, concinnat linguam mendacii.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Dolus in corde cogitantium mala: qui autem pacis ineunt consilia, sequitur eos gaudium.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Non contristabit iustum quidquid ei acciderit: impii autem replebuntur malo.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Abominatio est Domino labia mendacia: qui autem fideliter agunt, placent ei.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Homo versatus celat scientiam: et cor insipientium provocat stultitiam.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
Manus fortium dominabitur: quæ autem remissa est, tributis serviet.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Mœror in corde viri humiliabit illum, et sermone bono lætificabitur.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Qui negligit damnum propter amicum, iustus est: iter autem impiorum decipiet eos.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Non inveniet fraudulentus lucrum: et substantia hominis erit auri pretium.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
In semita iustitiæ, vita: iter autem devium ducit ad mortem.

< Mithali 12 >