< Mithali 12 >
1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Chi ama la disciplina ama la scienza, chi odia la correzione è stolto.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Il buono si attira il favore del Signore, ma egli condanna l'intrigante.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Non resta saldo l'uomo con l'empietà, ma la radice dei giusti non sarà smossa.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
La donna perfetta è la corona del marito, ma quella che lo disonora è come carie nelle sue ossa.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
I pensieri dei giusti sono equità, i propositi degli empi sono frode.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Le parole degli empi sono agguati sanguinari, ma la bocca degli uomini retti vi si sottrarrà.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Gli empi, una volta abbattuti, più non sono, ma la casa dei giusti sta salda.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Un uomo è lodato per il senno, chi ha un cuore perverso è disprezzato.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Un uomo di poco conto che basta a se stesso vale più di un uomo esaltato a cui manca il pane.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Il giusto ha cura del suo bestiame, ma i sentimenti degli empi sono spietati.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Chi coltiva la sua terra si sazia di pane, chi insegue chimere è privo di senno.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Le brame dell'empio sono una rete di mali, la radice dei giusti produce frutti.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Nel peccato delle sue labbra si impiglia il malvagio, ma il giusto sfuggirà a tale angoscia.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Ognuno si sazia del frutto della sua bocca, ma ciascuno sarà ripagato secondo le sue opere.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Lo stolto giudica diritta la sua condotta, il saggio, invece, ascolta il consiglio.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Lo stolto manifesta subito la sua collera, l'accorto dissimula l'offesa.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Chi aspira alla verità proclama la giustizia, il falso testimone proclama l'inganno.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
V'è chi parla senza riflettere: trafigge come una spada; ma la lingua dei saggi risana.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
La bocca verace resta ferma per sempre, la lingua bugiarda per un istante solo.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Amarezza è nel cuore di chi trama il male, gioia hanno i consiglieri di pace.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Al giusto non può capitare alcun danno, gli empi saranno pieni di mali.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Le labbra menzognere sono un abominio per il Signore che si compiace di quanti agiscono con sincerità.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
L'uomo accorto cela il sapere, il cuore degli stolti proclama la stoltezza.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
La mano operosa ottiene il comando, quella pigra sarà per il lavoro forzato.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
L'affanno deprime il cuore dell'uomo, una parola buona lo allieta.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Il giusto è guida per il suo prossimo, ma la via degli empi fa smarrire.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Il pigro non troverà selvaggina; la diligenza è per l'uomo un bene prezioso.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Nella strada della giustizia è la vita, il sentiero dei perversi conduce alla morte.