< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Celui qui aime l'instruction, aime la science; mais celui qui hait d'être repris, est un stupide.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
L'homme de bien attire la faveur de l'Eternel; mais [l'Eternel] condamnera l'homme qui machine du mal.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
L'homme ne sera point affermi par la méchanceté; mais la racine des justes ne sera point ébranlée.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
La femme vaillante est la couronne de son mari; mais celle qui fait honte, est comme de la vermoulure à ses os.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Les pensées des justes ne sont que jugement; mais les conseils des méchants ne sont que fraude.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Les paroles des méchants ne tendent qu'à dresser des embûches pour répandre le sang; mais la bouche des hommes droits les délivrera.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Les méchants sont renversés, et ils ne sont plus; mais la maison des justes se maintiendra.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
L'homme est loué selon sa prudence; mais le cœur dépravé sera en mépris.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Mieux vaut l'homme qui ne fait point cas de soi-même, bien qu'il ait des serviteurs, que celui qui se glorifie, et qui a faute de pain.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Le juste a égard à la vie de sa bête; mais les compassions des méchants sont cruelles.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Celui qui laboure sa terre, sera rassasié de pain; mais celui qui suit les fainéants, est dépourvu de sens.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Ce que le méchant désire, est un rets de maux; mais la racine des justes donnera [son fruit.]
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Il y a un lacet de mal dans le forfait des lèvres; mais le juste sortira de la détresse.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
L'homme sera rassasié de biens par le fruit de sa bouche; et on rendra à l'homme la rétribution de ses mains.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
La voie du fou est droite à son opinion; mais celui qui écoute le conseil, est sage.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Quant au fou, son dépit se connaît le même jour; mais l'homme bien avisé couvre son ignominie.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Celui qui prononce des choses véritables, fait rapport de ce qui est juste; mais le faux témoin fait des rapports trompeurs.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Il y a tel qui profère comme des pointes d'épée; mais la langue des sages est santé.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
La parole véritable est ferme à perpétuité; mais la fausse langue n'est que pour un moment.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Il y aura tromperie dans le cœur de ceux qui machinent du mal; mais il y aura de la joie pour ceux qui conseillent la paix.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
On ne fera point qu'aucun outrage rencontre le juste; mais les méchants seront remplis de mal.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Les fausses lèvres sont une abomination à l'Eternel; mais ceux qui agissent fidèlement, lui sont agréables.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
L'homme bien avisé cèle la science; mais le cœur des fous publie la folie.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
La main des diligents dominera; mais la main paresseuse sera tributaire.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Le chagrin qui est au cœur de l'homme, l'accable; mais la bonne parole le réjouit.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Le juste a plus de reste que son voisin; mais la voie des méchants les fera fourvoyer.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Le paresseux ne rôtit point sa chasse; mais les biens précieux de l'homme sont au diligent.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
La vie est dans le chemin de la justice, et la voie de son sentier ne tend point à la mort.

< Mithali 12 >