< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Celui qui aime la discipline aime la sagesse; celui qui hait les réprimandes est insensé.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Le meilleur est celui qui a trouvé la grâce du Seigneur; l'homme pervers tombera dans l'oubli.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
L'homme ne tire aucun profit de l'injustice; les racines des justes ne seront pas arrachées.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Une femme forte est une couronne pour son mari; comme un ver qui ronge le bois, une femme malfaisante perd son mari.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Les pensées des justes sont des sentences; les impies n'ont pour se gouverner que la ruse.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Les paroles des impies sont trompeuses; la bouche des hommes droits les sauvera.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Le jour où l'impie tombe, il est effacé; la maison des justes est inébranlable.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
On loue la bouche d'un homme intelligent; les esprits vains sont moqués.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Mieux vaut être obscur et utile à soi-même, que se glorifier en manquant de pain.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Le juste est compatissant, même pour la vie de ses bestiaux; les entrailles des impies sont sans pitié.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Qui travaille à sa terre se rassasiera de pain; mais ceux qui poursuivent des vanités sont dépourvus d'intelligence. Celui qui se plaît aux assemblées des buveurs léguera la honte à sa maison.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Les désirs des impies sont mauvais; les racines des hommes pieux sont indestructibles.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Par le péché même de ses lèvres, le pécheur tombe en des filets; le juste y échappe, et celui dont l'œil est bon excite l'indulgence; celui qui se dispute aux portes irrite les âmes.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
L'âme de l'homme sera remplie de biens provenant de sa bouche, et ses lèvres recevront leur récompense.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Les voies des insensés sont droites à leurs yeux; le sage écoute les conseils.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
L'insensé à l'instant même montre sa colère; l'homme habile renferme en lui-même l'outrage qu'il a reçu.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Le juste déclare la pleine vérité; le témoin des méchants est trompeur.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Il en est dont les paroles blessent comme des glaives; la langue des sages guérit.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Des lèvres véridiques n'ont point de détours sans leur témoignage; le témoin précipité a une langue inique.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
La fraude est dans le cœur de celui qui machine le mal; ceux qui veulent la paix seront dans la joie.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Rien d'injuste ne plaira au juste; les impies sont remplis de mal.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Les lèvres trompeuses sont en abomination au Seigneur; Il agrée l'homme de bonne foi.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
L'homme intelligent est un trône de science; le cœur des insensés ne rencontrera que malédictions.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
La main des élus aura sans peine la domination; les trompeurs seront livrés au pillage.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Les rumeurs sinistres troublent le cœur des justes; une bonne nouvelle les réjouit.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
L'arbitre équitable est ami de soi-même; les calamités poursuivront le pécheur, et la voie des impies les mènera aux égarements.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Le trompeur n'atteindra pas de proie; c'est une richesse précieuse que d'être pur.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Dans les voies de la justice est la vie; les voies des vindicatifs mènent à la mort.

< Mithali 12 >