< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Qui aime l’instruction aime la connaissance, et qui hait la répréhension est stupide.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
L’homme de bien obtient la faveur de par l’Éternel, mais l’homme qui fait des machinations, il le condamne.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
L’homme n’est point affermi par la méchanceté, mais la racine des justes n’est pas ébranlée.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Une femme vertueuse est la couronne de son mari, mais celle qui fait honte est comme de la pourriture dans ses os.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Les pensées des justes sont jugement, les desseins des méchants sont fraude.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Les paroles des méchants sont des embûches pour [verser] le sang, mais la bouche des hommes droits les délivrera.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Renversez les méchants, et ils ne sont plus; mais la maison des justes demeure.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Un homme est loué d’après sa prudence, mais le cœur perverti est en butte au mépris.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Mieux vaut celui qui est d’humble condition, et qui a un serviteur, que celui qui fait l’important et qui manque de pain.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Le juste regarde à la vie de sa bête, mais les entrailles des méchants sont cruelles.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Celui qui laboure sa terre sera rassasié de pain, mais celui qui court après les fainéants est dépourvu de sens.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Le méchant désire la proie des mauvaises gens, mais la racine des justes est productive.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Il y a un mauvais piège dans la transgression des lèvres, mais le juste sort de la détresse.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Du fruit de sa bouche un homme est rassasié de biens, et on rendra à l’homme l’œuvre de ses mains.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
La voie du fou est droite à ses yeux, mais celui qui écoute le conseil est sage.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
L’irritation du fou se connaît le jour même, mais l’homme avisé couvre sa honte.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Celui qui dit la vérité annonce la justice, mais le faux témoin, la fraude.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Il y a tel homme qui dit légèrement ce qui perce comme une épée, mais la langue des sages est santé.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
La lèvre véridique est ferme pour toujours, mais la langue fausse n’est que pour un instant.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
La fraude est dans le cœur de ceux qui machinent le mal, mais il y a de la joie pour ceux qui conseillent la paix.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Aucun malheur n’arrive au juste, mais les méchants seront comblés de maux.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Les lèvres menteuses sont en abomination à l’Éternel, mais ceux qui pratiquent la fidélité lui sont agréables.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
L’homme avisé couvre la connaissance, mais le cœur des sots proclame la folie.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
La main des diligents dominera, mais la [main] paresseuse sera tributaire.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
L’inquiétude dans le cœur d’un homme l’abat, mais une bonne parole le réjouit.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Le juste montre le chemin à son compagnon, mais la voie des méchants les fourvoie.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Le paresseux ne rôtit pas sa chasse; mais les biens précieux de l’homme sont au diligent.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
La vie est dans le sentier de la justice, et il n’y a pas de mort dans le chemin qu’elle trace.

< Mithali 12 >