< Mithali 12 >
1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
to love: lover discipline to love: lover knowledge and to hate argument stupid
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
pleasant to promote acceptance from LORD and man plot be wicked
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
not to establish: establish man in/on/with wickedness and root righteous not to shake
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
woman: wife strength: worthy crown master: husband her and like/as rottenness in/on/with bone his be ashamed
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
plot righteous justice counsel wicked deceit
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
word wicked to ambush blood and lip upright to rescue them
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
to overturn wicked and nothing they and house: home righteous to stand: stand
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
to/for lip: according understanding his to boast: praise man and to twist heart to be to/for contempt
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
pleasant to dishonor and servant/slave to/for him from to honor: honour and lacking food: bread
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
to know righteous soul: life animal his and compassion wicked cruel
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
to serve: labour land: soil his to satisfy food: bread and to pursue worthless lacking heart
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
to desire wicked net bad: evil and root righteous to give: give
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
in/on/with transgression lips snare bad: evil and to come out: come from distress righteous
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
from fruit lip man to satisfy good and recompense hand man (to return: return *Q(K)*) to/for him
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
way: conduct fool(ish) upright in/on/with eye his and to hear: hear to/for counsel wise
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
fool(ish) in/on/with day: today to know vexation his and to cover dishonor prudent
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
to breathe faithfulness to tell righteousness and witness deception deceit
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
there to speak rashly like/as thrust sword and tongue wise healing
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
lips truth: true to establish: establish to/for perpetuity and till to disturb tongue deception
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
deceit in/on/with heart to plow/plot bad: evil and to/for to advise peace joy
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
not to meet to/for righteous all evil: trouble and wicked to fill bad: evil
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
abomination LORD lips deception and to make: do faithfulness acceptance his
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
man prudent to cover knowledge and heart fool to call: call out folly
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
hand sharp to rule (and slackness *L(bah)*) to be to/for taskworker
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
anxiety in/on/with heart man to bow her and word pleasant to rejoice her
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
to spy from neighbor his righteous and way: conduct wicked to go astray them
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
not to roast slackness wild game his and substance man precious sharp
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
in/on/with way righteousness life and way: road path not death