< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
At elske Tugt er at elske Kundskab, at hade Revselse er dumt.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Den gode vinder Yndest hos HERREN, den rænkefulde dømmer han skyldig.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Ingen staar fast ved Gudløshed, men retfærdiges Rod skal aldrig rokkes.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
En duelig Kvinde er sin Ægtemands Krone, en daarlig er som Edder i hans Ben.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Retfærdiges Tanker er Ret, gudløses Opspind er Svig.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Gudløses Ord er paa Lur efter Blod, retsindiges Mund skal bringe dem Frelse.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Gudløse styrtes og er ikke mer, retfærdiges Hus staar fast.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
For sin Klogskab prises en Mand, til Spot bliver den, hvis Vid er vrangt.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Hellere overses, naar man holder Træl, end optræde stort, naar man mangler Brød.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Den retfærdige føler med sit Kvæg, gudløses Hjerte er grumt.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Den mættes med Brød, som dyrker sin Jord, uden Vid er den, der jager efter Tomhed.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
De ondes Fæstning jævnes med Jorden, de retfærdiges Rod holder Stand.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
I Læbernes Brøde hildes den onde, den retfærdige undslipper Nøden.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Af sin Munds Frugt mættes en Mand med godt, et Menneske faar, som hans Hænder har øvet.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Daarens Færd behager ham selv, den vise hører paa Raad.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
En Daare giver straks sin Krænkelse Luft, den kloge spottes og lader som intet.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Den sanddru fremfører, hvad der er ret, det falske Vidne kommer med Svig.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Mangens Snak er som Sværdhug, de vises Tunge læger.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Sanddru Læbe bestaar for evigt, Løgnetunge et Øjeblik.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
De, som smeder ondt, har Svig i Hjertet; de, der stifter Fred, har Glæde.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Den retfærdige times der intet ondt, gudløse oplever Vanheld paa Vanheld.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Løgnelæber er HERREN en Gru, de ærlige har hans Velbehag.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Den kloge dølger sin Kundskab, Taabers Hjerte udraaber Daarskab.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
De flittiges Haand skal raade, den lade tvinges til Hoveriarbejde.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Hjertesorg bøjer til Jorden, et venligt Ord gør glad.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Den retfærdige vælger sin Græsgang, gudløses Vej vildleder dem selv.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Ladhed opskræmmer intet Vildt, men kosteligt Gods faar den flittige tildelt.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Paa Retfærds Sti er der Liv, til Døden fører den onde Vej.

< Mithali 12 >