< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Kdo miluje cvičení, miluje umění; kdož pak nenávidí domlouvání, nemoudrý jest.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Dobrý nalézá lásku u Hospodina, ale muže nešlechetného potupí Bůh.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Nebývá trvánlivý člověk v bezbožnosti, kořen pak spravedlivých nepohne se.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Žena statečná jest koruna muže svého, ale jako hnis v kostech jeho ta, kteráž k hanbě přivodí.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Myšlení spravedlivých jsou pravá, rady pak bezbožných lstivé.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Slova bezbožných úklady činí krvi, ústa pak spravedlivých vytrhují je.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Vyvráceni bývají bezbožní tak, aby jich nebylo, ale dům spravedlivých ostojí.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Podlé toho, jakž rozumný jest, chválen bývá muž, převráceného pak srdce bude v pohrdání.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Lepší jest nevzácný, kterýž má služebníka, nežli ten, kterýž sobě slavně počíná, a nemá chleba.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Pečuje spravedlivý o život hovádka svého, srdce pak bezbožných ukrutné jest.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Kdo dělá zemi svou, nasycen bývá chlebem; ale kdož následuje zahalečů, blázen jest.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Žádostiv jest bezbožný obrany proti zlému, ale kořen spravedlivých způsobuje ji.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
Do přestoupení rtů zapletá se zlostník, ale spravedlivý vychází z ssoužení.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Z ovoce úst každý nasycen bude dobrým, a odplatu za skutky člověka dá jemu Bůh.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Cesta blázna přímá se zdá jemu, ale kdo poslouchá rady, moudrý jest.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Hněv blázna v tentýž den poznán bývá, ale opatrný hanbu skrývá.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Kdož mluví pravdu, ohlašuje spravedlnost, svědek pak falešný lest.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Někdo vynáší řeči podobné meči probodujícímu, ale jazyk moudrých jest lékařství.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Rtové pravdomluvní utvrzeni budou na věky, ale na kratičko jazyk lživý.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
V srdci těch, kteříž zlé obmýšlejí, bývá lest, v těch pak, kteříž radí ku pokoji, veselí.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Nepotká spravedlivého žádná těžkost, bezbožní pak naplněni budou zlým.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Ohavností jsou Hospodinu rtové lživí, ale ti, jenž činí pravdu, líbí se jemu.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Člověk opatrný tají umění, ale srdce bláznů vyvolává bláznovství.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
Ruka pracovitých panovati bude, lstivá pak musí dávati plat.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Starost v srdci člověka snižuje ji, ale věc dobrá obveseluje ji.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Vzácnější jest nad bližního svého spravedlivý, cesta pak bezbožných svodí je.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Nebude péci fortelný, což ulovil, ale člověk bedlivý statku drahého nabude.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Na stezce spravedlnosti jest život, a cesta stezky její nesmrtelná jest.

< Mithali 12 >