< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
EL peso falso abominación es á Jehová: mas la pesa cabal le agrada.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Cuando viene la soberbia, viene también la deshonra: mas con los humildes es la sabiduría.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
La integridad de los rectos los encaminará: mas destruirá á los pecadores la perversidad de ellos.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
No aprovecharán las riquezas en el día de la ira: mas la justicia librará de muerte.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
La justicia del perfecto enderezará su camino: mas el impío por su impiedad caerá.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
La justicia de los rectos los librará: mas los pecadores en su pecado serán presos.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Cuando muere el hombre impío, perece [su] esperanza; y la espectativa de los malos perecerá.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
El justo es librado de la tribulación: mas el impío viene en lugar suyo.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
El hipócrita con la boca daña á su prójimo: mas los justos son librados con la sabiduría.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
En el bien de los justos la ciudad se alegra: mas cuando los impíos perecen, hay fiestas.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
Por la bendición de los rectos la ciudad será engrandecida: mas por la boca de los impíos ella será trastornada.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
El que carece de entendimiento, menosprecia á su prójimo: mas el hombre prudente calla.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
El que anda en chismes, descubre el secreto: mas el de espíritu fiel encubre la cosa.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Cuando faltaren las industrias, caerá el pueblo: mas en la multitud de consejeros hay salud.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Con ansiedad será afligido el que fiare al extraño: mas el que aborreciere las fianzas [vivirá] confiado.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
La mujer graciosa tendrá honra: y los fuertes tendrán riquezas.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
A su alma hace bien el hombre misericordioso: mas el cruel atormenta su carne.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
El impío hace obra falsa: mas el que sembrare justicia, tendrá galardón firme.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
Como la justicia [es] para vida, así el que sigue el mal [es] para su muerte.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Abominación son á Jehová los perversos de corazón: mas los perfectos de camino le son agradables.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
[Aunque llegue] la mano á la mano, el malo no quedará sin castigo: mas la simiente de los justos escapará.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Zarcillo de oro en la nariz del puerco, [es] la mujer hermosa y apartada de razón.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
El deseo de los justos es solamente bien: [mas] la esperanza de los impíos es enojo.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Hay quienes reparten, y les es añadido más: y hay quienes son escasos más de lo que es justo, mas vienen á pobreza.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
El alma liberal será engordada: y el que saciare, él también será saciado.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Al que retiene el grano, el pueblo lo maldecirá: mas bendición será sobre la cabeza del que vende.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
El que madruga al bien, buscará favor: mas el que busca el mal, vendrále.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
El que confía en sus riquezas, caerá: mas los justos reverdecerán como ramos.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
El que turba su casa heredará viento; y el necio será siervo del sabio de corazón.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
El fruto del justo es árbol de vida: y el que prende almas, es sabio.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Ciertamente el justo será pagado en la tierra: ¡cuánto más el impío y el pecador!

< Mithali 11 >