< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
A balança enganosa [é] abominação ao SENHOR; mas o peso justo [é] seu prazer.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Quando vem a arrogância, vem também a desonra; mas com os humildes [está] a sabedoria.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
A integridade dos corretos os guia; mas a perversidade dos enganadores os destruirá.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Nenhum proveito terá a riqueza no dia da ira; mas a justiça livrará da morte.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
A justiça do íntegro endireitará seu caminho; mas o perverso cairá por sua perversidade.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
A justiça dos corretos os livrará; mas os transgressores serão presos em sua própria perversidade.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Quando o homem mau morre, sua expectativa morre; e a esperança de seu poder perece.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
O justo é livrado da angústia; e o perverso vem em seu lugar.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
O hipócrita com a boca prejudica ao seu próximo; mas os justos por meio do conhecimento são livrados.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
No bem dos justos, a cidade se alegra muito; e quando os perversos perecem, há alegria.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
Pelo bênção dos sinceros a cidade se exalta; mas pela boca dos perversos ela se destrói.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
Aquele que não tem entendimento despreza a seu próximo; mas o homem bom entendedor se mantêm calado.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
Aquele que conta fofocas revela o segredo; mas o fiel de espírito encobre o assunto.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Quando não há conselhos sábios, o povo cai; mas na abundância de bons conselheiros [consiste] o livramento.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Certamente aquele que se tornar fiador de algum estranho passará por sofrimento; mas aquele odeia firmar compromissos [ficará] seguro.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
A mulher graciosa guarda a honra, assim como os violentos guardam as riquezas.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
O homem bondoso faz bem à sua alma; mas o cruel atormenta sua [própria] carne.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
O perverso recebe falso pagamento; mas aquele que semeia justiça [terá] uma recompensa fiel.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
Assim como a justiça [leva] para a vida; assim também aquele que segue o mal [é levado] para sua [própria] morte.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
O SENHOR abomina os perversos de coração; porém ele se agrada que caminham com sinceridade.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Com certeza o mal não será absolvido; mas a semente dos justos escapará livre.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
A mulher bela mas sem discrição é como uma joia no focinho de uma porca.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
O desejo dos justos é somente para o bem; mas a esperança dos perversos é a fúria.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Há quem dá generosamente e tem cada vez mais; e há quem retém mais do que é justo e empobrece.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
A alma generosa prosperará, e aquele que saciar também será saciado.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
O povo amaldiçoa ao que retém o trigo; mas bênção haverá sobre a cabeça daquele que [o] vende.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
Aquele que com empenho busca o bem, busca favor; porém o que procura o mal, sobre ele isso lhe virá.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Aquele que confia em suas riquezas cairá; mas os justos florescerão como as folhas.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
Aquele que perturba sua [própria] casa herdará vento; e o tolo será servo do sábio de coração.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
O fruto do justo é uma árvore de vida; e o que ganha almas é sábio.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Ora, se o justo recebe seu pagamento na terra, quanto mais o perverso e o pecador!

< Mithali 11 >