< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
Balança enganosa é abominação ao Senhor, mas o peso justo o seu prazer.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Vinda a soberba, virá também a afronta; mas com os humildes está a sabedoria.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
A sinceridade dos sinceros os encaminhará, mas a perversidade dos aleives os destruirá.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Não aproveitam as riquezas no dia da indignação, mas a justiça livra da morte.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
A justiça do sincero endireitará o seu caminho, mas o ímpio pela sua impiedade cairá.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
A justiça dos virtuosos os livrará, mas na sua perversidade serão apanhados os iníquos.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Morrendo o homem ímpio perece a sua expectação, e a esperança dos injustos se perde.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
O justo é livre da angústia, e o ímpio vem em seu lugar.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
O hipócrita com a boca destrói ao seu companheiro, mas os justos são livres pelo conhecimento.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
No bem dos justos exulta a cidade; e, perecendo os ímpios, há júbilo.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
Pela benção dos sinceros se exalta a cidade, mas pela boca dos ímpios se derriba.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
O que carece de entendimento despreza a seu companheiro, mas o homem bem entendido cala-se.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
O que anda praguejando descobre o segredo, mas o fiel de espírito encobre o negócio.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Não havendo sábios conselhos, o povo cai, mas na multidão de conselheiros há segurança.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Decerto sofrerá severamente aquele que fica por fiador do estranho, mas o que aborrece aos que dão as mãos estará seguro.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
A mulher aprazível guarda a honra, como os violentos guardam as riquezas.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
O homem benigno faz bem à sua própria alma, mas o cruel perturba a sua própria carne.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
O ímpio faz obra falsa, mas para o que semeia justiça haverá galardão fiel.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
Como a justiça encaminha para a vida, assim o que segue o mal vai para a sua morte.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Abominação são ao Senhor os perversos de coração, mas os sinceros de caminho são o seu deleite.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Ainda que o mau junte mão à mão, não será inculpável, mas a semente dos justos escapará.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Como jóia de ouro na tromba da porca, assim é a mulher formosa, que se aparta da razão.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
O desejo dos justos tão somente é o bem, mas a esperança dos ímpios é a indignação.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Alguns há que espalham, e ainda se lhes acrescenta mais, e outros que reteem mais do que é justo, mas é para a sua perda.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
A alma abençoante engordará, e o que regar, ele também será regado.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Ao que retém o trigo o povo amaldiçoa, mas benção haverá sobre a cabeça do vendedor:
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
O que busca cedo o bem busca favor, porém o que procura o mal a esse lhe sobrevirá.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Aquele que confia nas suas riquezas cairá, mas os justos reverdecerão como a rama.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
O que perturba a sua casa herdará o vento, e o tolo será servo do entendido de coração.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
O fruto do justo é árvore de vida, e o que ganha almas sábio é.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Eis que o justo é recompensado na terra; quanto mais o será o ímpio e o pecador.

< Mithali 11 >