< Mithali 11 >
1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
Les balances fausses sont en abomination au Seigneur; le poids juste Lui est agréable.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Où est l'orgueil, il y aura confusion; la bouche des humbles s'exercent à la sagesse.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
Le juste en mourant laisse des regrets; la mort des impies cause l'indifférence ou la joie.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
L'équité trace des voies irréprochables; l'impiété trébuche contre l'injustice.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
L'équité des hommes droits les sauve; les pervers sont pris dans leur propre perdition.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
L'espérance des justes ne meurt pas avec eux; l'orgueil des impies ne leur survit point.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
Le juste échappe aux chasseurs d'hommes; à sa place, l'impie leur est livré.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
La bouche de l'impie tend un piège aux citoyens; l'intelligence du juste les guide dans la bonne voie.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
Grâce aux justes, une cité prospère;
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
au contraire, elle est renversée par la bouche des impies.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
L'insensé se joue des citoyens; un homme prudent ramène le calme.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
L'homme à la langue double divulgue les conseils de l'assemblée; l'homme fidèle garde le secret sur les affaires.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Ceux qui n'ont point de gouvernail tombent comme des feuilles. Le salut réside dans une grande puissance.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Le méchant fait le mal, même quand il se rapproche du juste; il n'aime pas son renom de fermeté.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
La femme gracieuse fait la gloire de son mari; la femme qui hait la justice est un trône de déshonneur. Les paresseux manquent de richesses; les forts travaillent à en amasser.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
L'homme charitable fait du bien à son âme; l'homme sans pitié perd son corps.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
L'impie fait des œuvres iniques; la race des justes recueille la récompense de la vérité.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
Un fils juste est né pour la vie; ce que poursuit l'impie mène à la mort.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Les voies tortueuses sont en abomination au Seigneur; mais Il agrée tous ceux qui sont irréprochables dans leurs voies.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Celui qui, dans une pensée injuste, met sa main dans la main d'autrui ne sera point impuni; au contraire, qui sème la justice en récoltera le digne salaire.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Tel est un pendant d'oreille au museau d'une truie; telle est la beauté chez la femme sans sagesse.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
Le désir du juste est bon sans réserve; l'espérance des impies périra.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Il en est qui, en distribuant leurs biens, les augmentent; il en est qui, même en s'amusant, s'appauvrissent.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
Toute âme simple est bénie; l'homme irascible n'est pas honoré.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Que celui qui amasse du blé le tienne en réserve pour les peuples; la bénédiction est sur la tête de celui qui en fait part à autrui.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
Celui qui médite le bien cherche une grâce salutaire; celui qui songe au mal le recueillera pour lui-même.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Celui qui se fie en sa richesse tombera; celui qui s'attache aux choses justes fleurira.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
Celui qui ne s'occupe pas de sa propre maison n'aura que le vent pour héritage; l'insensé sera le serviteur du sage.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
Du fruit de la justice naît l'arbre de vie; les âmes des pervers seront emportées avant le temps.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Si le juste est difficilement sauvé, que penser de l'impie et du pécheur?