< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
La balance fausse est en horreur à Yahweh, mais le poids juste lui est agréable.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Si l'orgueil vient, viendra aussi l'ignominie; mais la sagesse est avec les humbles.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
L'innocence des hommes droits les dirige, mais les détours des perfides les ruinent.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Au jour de la colère, la richesse ne sert de rien, mais la justice délivre de la mort.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
La justice de l'homme intègre dirige ses voies, mais le méchant tombe par sa méchanceté.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
La justice des hommes droits les délivre, mais les perfides sont pris par leur propre malice.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Quand meurt le méchant, son espoir périt, et l'attente du pervers est anéantie.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
Le juste est délivré de l'angoisse, et le méchant y tombe à sa place.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
Par sa bouche l'impie prépare la ruine de son prochain, mais les justes seront délivrés par la science.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
Quand les justes sont heureux, la ville se réjouit; quand les méchants périssent, on pousse des cris de joie.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
Par la bénédiction des hommes droits la ville prospère; elle est renversée par la bouche des impies.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
Celui qui méprise son prochain est dépourvu de sens, mais l'homme intelligent se tait.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
Le médisant dévoile les secrets, mais l'homme au cœur fidèle tient la chose cachée.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Quand la direction fait défaut, le peuple tombe; le salut est le grand nombre des conseillers.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Qui cautionne un inconnu s'en repent, mais celui qui craint de s'engager est en sécurité.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
La femme qui a de la grâce obtient la gloire, les hommes énergiques acquièrent la richesse.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
L'homme charitable fait du bien à son âme, mais l'homme cruel afflige sa propre chair.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
Le méchant fait un travail trompeur, mais celui qui sème la justice a une récompense assurée.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
La justice conduit à la vie, mais celui qui poursuit le mal va à la mort.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Les hommes au cœur pervers sont en abomination à Yahweh, mais ceux qui sont intègres en leur voie sont l'objet de ses complaisances.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Non, le méchant ne restera pas impuni, mais la postérité des justes sera sauvée.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Un anneau d'or au nez d'un pourceau, telle est la femme belle et dépourvue de sens.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
Le désir des justes, c'est uniquement le bien; l'attente des méchants, c'est la fureur.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Celui-ci donne libéralement et s'enrichit; cet autre épargne outre mesure et s'appauvrit.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
L'âme bienfaisante sera rassasiée, et celui qui arrose sera lui-même arrosé.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Celui qui retient le blé est maudit du peuple, mais la bénédiction est sur la tête de celui qui le vend.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
Celui qui recherche le bien trouve la faveur, mais celui qui cherche le mal, le mal l'atteindra.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Celui qui se confie dans sa richesse tombera, mais les justes germeront comme le feuillage.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
Celui qui trouble sa maison héritera le vent, et l'insensé sera l'esclave de l'homme sage.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
Le fruit du juste est un arbre de vie, et qui fait la conquête des âmes est sage.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Si le juste reçoit sur la terre une rétribution de peines, combien plus le méchant et le pécheur!

< Mithali 11 >