< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
balance deceit abomination LORD and stone: weight complete acceptance his
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
to come (in): come arrogance and to come (in): come dishonor and with humble wisdom
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
integrity upright to lead them and crookedness to act treacherously (to ruin them *Q(K)*)
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
not to gain substance in/on/with day fury and righteousness to rescue from death
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
righteousness unblemished: blameless to smooth way: conduct his and in/on/with wickedness his to fall: fall wicked
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
righteousness upright to rescue them and in/on/with desire to act treacherously to capture
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
in/on/with death man wicked to perish hope and hope strength to perish
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
righteous from distress to rescue and to come (in): come wicked underneath: instead him
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
in/on/with lip profane to ruin neighbor his and in/on/with knowledge righteous to rescue
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
in/on/with goodness righteous to rejoice town and in/on/with to perish wicked cry
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
in/on/with blessing upright to exalt town and in/on/with lip wicked to overthrow
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
to despise to/for neighbor his lacking heart and man understanding be quiet
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
to go: went slander to reveal: reveal counsel and be faithful spirit to cover word: thing
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
in/on/with nothing counsel to fall: fall people and deliverance: victory in/on/with abundance to advise
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
bad: evil be evil for to pledge be a stranger and to hate to blow to trust
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
woman favor to grasp glory and ruthless to grasp riches
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
to wean soul: myself his man kindness and to trouble flesh his cruel
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
wicked to make: do wages deception and to sow righteousness hire truth: certain
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
right righteousness to/for life and to pursue distress: evil to/for death his
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
abomination LORD twisted heart and acceptance his unblemished: blameless way: conduct
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
hand: to to/for hand: certainly not to clear bad: evil and seed: children righteous to escape
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
ring gold in/on/with face: nose swine woman beautiful and to turn aside: remove taste
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
desire righteous surely good hope wicked fury
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
there to scatter and to add still and to withhold from uprightness surely to/for need
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
soul: myself blessing to prosper and to quench also he/she/it to shoot
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
to withhold grain to curse him people and blessing to/for head to buy grain
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
to seek good to seek acceptance and to seek distress: evil to come (in): come him
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
to trust in/on/with riches his he/she/it to fall: fall and like/as leaf righteous to sprout
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
to trouble house: household his to inherit spirit: breath and servant/slave fool(ish) to/for wise heart
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
fruit righteous tree life and to take: take soul wise
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
look! righteous in/on/with land: country/planet to complete also for wicked and to sin

< Mithali 11 >