< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
A false balance is abomination to the LORD: but a just weight is his delight.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
When pride comes, then comes shame: but with the lowly is wisdom.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
The integrity of the upright shall guide them: but the perverseness of transgressors shall destroy them.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Riches profit not in the day of wrath: but righteousness delivers from death.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
The righteousness of the perfect shall direct his way: but the wicked shall fall by his own wickedness.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
The righteousness of the upright shall deliver them: but transgressors shall be taken in their own naughtiness.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
When a wicked man dies, his expectation shall perish: and the hope of unjust men perishes.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
The righteous is delivered out of trouble, and the wicked comes in his stead.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
An hypocrite with his mouth destroys his neighbor: but through knowledge shall the just be delivered.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
When it goes well with the righteous, the city rejoices: and when the wicked perish, there is shouting.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
By the blessing of the upright the city is exalted: but it is overthrown by the mouth of the wicked.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
He that is void of wisdom despises his neighbor: but a man of understanding holds his peace.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
A talebearer reveals secrets: but he that is of a faithful spirit conceals the matter.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Where no counsel is, the people fall: but in the multitude of counsellors there is safety.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
He that is surety for a stranger shall smart for it: and he that hates indebtedness is sure.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
A gracious woman retains honor: and strong men retain riches.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
The merciful man does good to his own soul: but he that is cruel troubles his own flesh.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
The wicked works a deceitful work: but to him that sows righteousness shall be a sure reward.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
As righteousness tends to life: so he that pursues evil pursues it to his own death.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
They that are of a fraudulent heart are abomination to the LORD: but such as are upright in their way are his delight.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Though hand join in hand, the wicked shall not be unpunished: but the seed of the righteous shall be delivered.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
As a jewel of gold in a swine’s snout, so is a fair woman which is without discretion.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
The desire of the righteous is only good: but the expectation of the wicked is wrath.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
There is that scatters, and yet increases; and there is that withholds more than is meet, but it tends to poverty.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
The liberal soul shall be made fat: and he that waters shall be watered also himself.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
He that withholds corn, the people shall curse him: but blessing shall be on the head of him that sells it.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
He that diligently seeks good procures favor: but he that seeks mischief, it shall come to him.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
He that trusts in his riches shall fall; but the righteous shall flourish as a branch.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
He that troubles his own house shall inherit the wind: and the fool shall be servant to the wise of heart.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
The fruit of the righteous is a tree of life; and he that wins souls is wise.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Behold, the righteous shall be recompensed in the earth: much more the wicked and the sinner.

< Mithali 11 >