< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
Falske Vægtskåle er HERREN en gru, fuldvvægtigt Lod er efter hans Sind.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
Kommer Hovmod, kommer og Skændsel, men med ydmyge følger der Visdom.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
Retsindiges Uskyld leder dem trygt, troløses falskhed lægger dem øde.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Ej hjælper Rigdom på Vredens Dag, men Retfærd redder fra Døden.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
Den lydefris Retfærd jævner hans Vej, for sin Gudløshed falder den gudløse.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
Retsindiges Retfærd bringer dem Frelse, troløse fanges i egen Attrå.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Ved Døden brister den gudløses Håb, Dårers Forventning brister.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
Den retfærdige fries af Trængsel, den gudløse kommer i hans Sted.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
Med sin Mund lægger vanhellig Næsten øde, retfærdige fries ved Kundskab.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
Ved retfærdiges Lykke jubler en By, der er Fryd ved gudløses Undergang.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
Ved retsindiges Velsignelse rejser en By sig, den styrtes i Grus ved gudløses Mund.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
Mand uden Vid ser ned på sin Næste, hvo, som har Indsigt, tier.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
Bagtaleren røber, hvad ham er betroet, den pålidelige skjuler Sagen.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Uden Styre står et Folk for Fald, vel står det til, hvor mange giver Råd.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Den går det ilde, som borger for andre, tryg er den, der hader Håndslag.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
Yndefuld Kvinde vinder Manden Ære; hader hun Retsind, volder hun Skændsel. De lade må savne Gods, flittige vinder sig Rigdom.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
Kærlig Mand gør vel mod sin Sjæl, den grumme er hård ved sit eget Kød.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
Den gudløse skaber kun skuffende Vinding, hvo Retfærd sår, får virkelig Løn.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
At hige efter Retfærd er Liv, at jage efter ondt er Død.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
De svigefulde er HERREN en Gru, hans Velbehag ejer, hvo lydefrit vandrer.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
Visselig undgår den onde ej Straf, de retfærdiges Æt går fri.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Som Guldring i Svinetryne er fager Kvinde, der ikke kan skønne.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
Retfærdiges Ønske bliver kun til Lykke, gudløse har kun Vrede i Vente.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
En strør om sig og gør dog Fremgang, en anden nægter sig alt og mangler.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
Gavmild Sjæl bliver mæt; hvo andre kvæger, kvæges og selv.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Hvo Kornet gemmer, ham bander Folket, Velsignelse kommer over den, som sælger.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
Hvo der jager efter godt, han søger efter Yndest, hvo der higer efter ondt, ham kommer det over.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Hvo der stoler på sin Rigdom, falder, retfærdige grønnes som Løv.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
Den, der øder sit Hus, høster Vind, Dåre bliver Vismands Træl.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
Retfærds Frugt er et Livets Træ, Vismand indfanger Sjæle.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
En retfærdig reddes med Nød og næppe, endsige en gudløs, en, der synder.

< Mithali 11 >