< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
上主深惡假秤,卻喜愛法碼準確。
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
傲慢來到,恥辱隨後而至;智慧只與謙遜人相處。
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
正直的人,以正義為領導;背義的人,必為邪惡所毀滅。
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
在上主盛怒之日,財富毫無用途;只有正義,能救人免於死亡。
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
完人的正義,為他修平道路;惡人必因自己的邪惡而顛仆。
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
正直的人,將因自己的正義而獲救;奸詐的人,反為自己的惡計所連累。
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
惡人一死,他的希望盡成泡影;同樣,奸匪的期待也全然消失。
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
義人得免患難,惡人反來頂替。
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
假善人以口舌,傷害自己的近人;義人因有知識,卻得以保全。
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
幾時義人幸運,全城歡騰;幾時惡人滅亡,歡聲四起。
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
義人的祝福,使城市興隆;惡人的口舌,使城市傾覆。
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
嘲弄自己朋友的人,毫無識趣;有見識的人,必沉默寡言。
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
往來傳話的人,必洩露秘密;心地誠樸的人,方能不露實情。
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
人民缺乏領導,勢必衰弱;人民的得救,正在於謀士眾多。
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
為外人作保的,必自討苦吃;厭惡作保的,必自享安全。
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
淑德的婦女,必為丈夫取得光榮;惱恨正義的婦女,正是一恥辱的寶座;懶散的人失落自己的財物,勤謹的人反取得財富。
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
為人慈善,是造福己身;殘酷的人,反自傷己命。
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
惡人所賺得的工資,是空虛的;播種正義者的報酬,纔是真實的。
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
恒行正義,必走向生命;追求邪惡,必自趨喪亡。
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
上主憎惡心邪的人,喜悅舉止無瑕的人。
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
惡人始終不能逃避懲罰,義人的後裔必獲得拯救。
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
女人美麗而不精明,猶如套在豬鼻上的金環。
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
義人的心願必獲善報;惡人的希望終歸破滅。
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
有人慷慨好施,反更富有;有人過於吝嗇,反更貧窮。
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
慈善為懷的人,必得富裕;施惠於人的人,必蒙施惠。
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
屯積糧食的人,必受人民咀咒;祝福卻降在賣糧食者的頭上。
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
慕求美善的,必求得恩寵;追求邪惡的,邪惡必臨其身。
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
信賴自己財富的人,必至衰落;義人卻茂盛有如綠葉。
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
危害自己家庭的,必承受虛幻;愚昧的人,必作心智者的奴隸。
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
義人的果實是生命樹,智慧的人能奪取人心。
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
看義人在地上還遭受報復,惡人和罪人更將如何﹖

< Mithali 11 >