< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Los proverbios de Salomón. Un hijo sabio hace un padre feliz; pero un hijo insensato trae dolor a su madre.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Los tesoros de la maldad no aprovechan nada, pero la justicia libra de la muerte.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Yahvé no permitirá que el alma del justo pase hambre, pero aleja el deseo de los malvados.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Se hace pobre el que trabaja con mano perezosa, pero la mano del diligente trae riqueza.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
El que recoge en verano es un hijo sabio, pero el que duerme durante la cosecha es un hijo que causa vergüenza.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Las bendiciones están en la cabeza de los justos, pero la violencia cubre la boca de los malvados.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
La memoria de los justos es bendita, pero el nombre de los malvados se pudrirá.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Los sabios de corazón aceptan los mandamientos, pero un tonto parlanchín caerá.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
El que camina sin culpa, camina con seguridad, pero el que pervierte sus caminos será descubierto.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
El que guiña el ojo causa dolor, pero un tonto parlanchín caerá.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La boca del justo es un manantial de vida, pero la violencia cubre la boca de los malvados.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
El odio suscita conflictos, pero el amor cubre todos los males.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
La sabiduría se encuentra en los labios del que tiene discernimiento, pero la vara es para la espalda del que no tiene entendimiento.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Los sabios acumulan conocimientos, pero la boca del necio está cerca de la ruina.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
La riqueza del rico es su ciudad fuerte. La destrucción de los pobres es su pobreza.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
El trabajo de los justos conduce a la vida. El aumento de los malvados lleva al pecado.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Está en el camino de la vida quien hace caso a la corrección, pero el que abandona la reprensión extravía a los demás.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
El que oculta el odio tiene labios mentirosos. El que profiere una calumnia es un necio.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
En la multitud de palabras no falta la desobediencia, pero el que refrena sus labios lo hace con sabiduría.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
La lengua del justo es como la plata selecta. El corazón de los malvados es de poco valor.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Los labios de los justos alimentan a muchos, pero los necios mueren por falta de entendimiento.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
La bendición de Yahvé trae riqueza, y no le añade ningún problema.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
El placer del necio es hacer la maldad, pero la sabiduría es un hombre de placer del entendimiento.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Lo que los malvados temen los alcanzará, pero el deseo de los justos será concedido.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Cuando el torbellino pasa, el malvado ya no existe; pero los justos se mantienen firmes para siempre.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Como vinagre a los dientes y como humo a los ojos, así es el perezoso para los que lo envían.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
El temor a Yahvé prolonga los días, pero los años de los impíos serán acortados.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
La perspectiva de los justos es la alegría, pero la esperanza de los malvados perecerá.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
El camino de Yahvé es una fortaleza para los rectos, sino que es una destrucción para los obreros de la iniquidad.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Los justos nunca serán eliminados, pero los malvados no habitarán la tierra.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
La boca del justo produce sabiduría, pero la lengua perversa será cortada.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Los labios de los justos saben lo que es aceptable, pero la boca de los malvados es perversa.

< Mithali 10 >